Habari kuhusu Singapore
Ripoti ya UNESCO kuhusu vyombo vya habari vya Singapore
Repoti ya Unesco inaonesha ‘udhibiti wa hali juu’ wa vyombo vikuu vya habari nchini Singapore huku ikizitambua blogu na tovuti za vyombo vyauanahabari mpya kuwa vinatoa “mazungumzo makini mbadala juu ya masuala muhimu ya kisiasa na jamii kama vile siasa za ndani ya nchi, haki za mashoga na wazee.”
Singapore: Wanablogu Waikosoa Ilani ya PAP
Chama kinachotawala Singapore, People’s Action Party (PAP), kilitoa ilani yake ya uchaguzi tarehe 17 aprili, 2011, ambayo mara moja ilikosolewa na wanablogu wengi kwa “kutokuwa wazi”. PAP tayari kimekuwa madarakani kwa miongo mitano. Uchaguzi mkuu nchini humo umefanyika tarehe 7 Mei.
Udhibiti Nchini Singapore
Singapore imesababisha kelele kubwa baada ya kupiga marufuku filamu ya aliyewahi kuwa mfungwa wa kisiasa na kumkamata mtunzi Mwingereza wa kitabu kilichoandiaka kuhusu adhabu ya kifo nchini humo. Wanablogu wanajadili.
Singapore: Kampeni ya “Kataa Ubakaji”
Nchini Singapore, mara nyingi kumbaka mke wako hakuchukuliwi kama tendo la kubaka. Waandaji wa kampeni ya “Kataa Ubakaji” wanataka kukomesha sheria inayokinga ubakaji ndani ya ndoa kwa kuzindua kampeni ya kukusanya saini ambazo zitawasilishwa kwa watunga sera. Wengi wa raia wa mtandaoni wanaiunga mkono kampeni hii.
Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu
Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.