Habari kuhusu Ufilipino
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia
Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.
Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu
Mvua kubwa ilisababisha mafuriko katika vitongoji vingi ya jiji la Manila pamoja na majimbo ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Mhariri wa Global Voices aliye huko Manila, Mong Palatino, anakusanya picha kutoka katika majukwaa mbalimbali ya habari za kiraia yanayoonyesha athari kubwa ya mafuriko hayo katika mji huo mkuu wa nchi.
Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011
Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011
Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV
Baadhi ya habari za kuvutia za Global Voices na video za hivi karibuni kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, Mashariki na Ulaya Kati, Karibeani pamoja na Marekani ya Kusini, zimeletwa na Juliana Rincón Parra.
Ufilipino: Maoni ya Wanablog Juu ya Elimu ya Ya afya ya Uzazi
Mwaka huu wa masomo serikali ya Philippines inatekeleza mpango wa elimu ya uzazi kwenye shule za umma unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na vijana. Na wanablogu wametoa maoni juu ya suala hilo.
Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao
Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.
Philippines: “Muswada wa Mkataba wa Ndoa Jadidifu”
Kikundi kimoja cha masuala maalum ya jamii nchini Philippines kinataka kuwasilisha sheria ambayo itaufanya mkataba wa ndoa kuwa na nguvu kwa miaka kumi tu. Pendekezo hilo la kipekee limezua mjadala mkali kwenye ulimwengu wa blogu.
Philippines: Mti wa Dita Waokoa Maisha ya Watu 36 Wakati wa Mafuriko
Mti wa aina ya Dita huko Manila mjini uligeuka kuwa "Mti wa Uzima" wakati ulipotumika kama kimbilio na wakazi ambao walitegwa kwenye nyumba zao wakati wa janga la kimbunga na mafuriko ya hivi karibuni. Somo: Usikate miti.
Uanaharakati na Umama Barani Asia
Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.
Philippines:Mafuriko Mabaya Zaidi Katika Kipindi cha Miaka 40
Kimbunga kilichopewa jina la 'Ondoy" kimeikumba Philippines jumamosi iliyopita na kusababisha mafuriko mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 ambayo yamesababisha vifo vya watu 50 na kusababisha wakazi 280, 000 kupoteza makazi. Tovuti za kijamii zilipashana habari za kimbunga hicho na jinsi ya kuwasaidia walioathirika.