Habari kuhusu Indonesia

Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia

Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.

4 Mei 2013

Indonesia: Maandamano ya Kupinga Bei ya Mafuta Yatikisha Majiji

Miji kadhaa ya nchini Indonesia iligubikwa na maandamano na vurugu za kupinga ongezeko la bei ya mafuta ya petroli katika wiki chache zilizopita. Wanahabari za mtandaoni walijadiliana ikiwa ongezeko hilo la bei lilikuwa jambo sahihi. Watumiaji wa Twita waliongeza nguvu ya wavuti wa kublogu ili kurusha taarifa za mapambano kati ya polisi na wanafunzi jijini Jakarta.

15 Aprili 2012

Indonesia: Sony yamkabili Sony

Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.

11 Aprili 2010

Indonesia: Sarafu za Kudai Haki

Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.

8 Disemba 2009

Tamasha la Blogu Indonesia

Tulitembelea tamasha la blogu la Indonesia au PestaBlogger 2009. Hii nim ara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika. Tukio hili lilishuhudia wanablogu kutoka kila sehemu ya Kisiwa hiki ambacho pia ni Taifa wakimiminika mjini Jakarta ili kusherehekea, kujadili na kujumuika.

6 Novemba 2009

Clinton Azuru Indonesia

Pamoja na kukutana na viongozi wa Indonesia, Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton alipata muda wa kutembelea makazi ya watu masikini mjini Jakarta. Kadhalika alitokea kwenye kipindi cha televisheni cha vijana. Ni nini maoni ya wanablogu?

26 Februari 2009

Indonesia: Talaka na Ndoa za Mitala

Najihisi nina hatia ninapoandika kuhusu talaka na ndoa za mitala wakati wa siku ya wapendanao ya Valentino. Lakini mada hizi zisizotamkika ni ukweli wa mapenzi na mahusiano. Katika Indonesia, wanawake wengi wanawataliki waume zao kwa sababu ya mitala.

22 Februari 2009