· Oktoba, 2008

Habari kuhusu China kutoka Oktoba, 2008

Macho ya Kimataifa kwenye Uchaguzi wa Marekani

Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wake wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya Collective Journalism inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices' Voices Without Votes (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.

Mwangwi wa Sakata la Maziwa China katika Afrika

  1 Oktoba 2008

Nchini China inakadiriwa kuwa watoto 13,000 wameugua tangu sakata la maziwa yasiyofaa kuibuka. Ushawishi na nguvu za China vimeongezeka Afrika, kama ulivyoongezeka uagizwaji wa bidhaa za kila namna, kuanzia viatu vya mazoezi mpaka chakula aina ya tambi. Mabloga hata wale walio mbali kama Kongo au Senegal, wanaguswa na usalama wa bidhaa za kutoka China katika nchi zao, na wanafuatilias habari hiyo (ya maziwa yasiyofaa).