Habari kuhusu Video kutoka Julai, 2013
Je, Ziara ya Obama Barani Afrika ni Neema au Hasara?
Rais wa Marekani Barack Obama amemaliza ziara yake ya siku sita katika nchi tatu za Kiafrika, Senegali, Afrika Kusini na Tanzania, mnamo Julai 2, 2013. Obama alitangaza mradi mpya, "Umeme Afrika", kukuza matumizi ya umeme mara dufu katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Maoni ya watu duniani kote juu ya umuhimu na matokeo ya ziara hiyo yamegawanyika mno.
Simulizi la Video [IsiyoHalisi] ya Kukamatwa kwa Morsi
Video inayoonyesha kile kinachoelezwa kuwa kukamatwa kwa rais wa zamani za Misri Mohamed Morsi inatembea sana mtandaoni hivi sasa. Video hiyo hiyo iliwekwa kwenye mtandao wa YouTube mnamo Mei 21, 2013 kwa kichwa cha habari "Wakati Rais Mohamed Morsi na mwanae walipokamatwa."