Habari kuhusu Video kutoka Mei, 2013
VIDEO: Namna Watu Wawili Tofauti Walivyopinga Dhuluma na Kushinda
Mkhuseli "Khusta" Jack na Oscar Olivera waliongoza harakati tofauti za kiraia zisizohusisha vurugu, moja ikiwa ni Afrika Kusini mwaka 1985 nyingine ikiwa ni Bolvia mwaka 2000. Video iliyoandaliwa na Shule ya Uandishi wa Weledi inasimulia habari zao
Mwandishi Habari za Kiraia wa Miaka 14 Auawa Akiripoti Mapigano Nchini Syria
Omar Qatifaan, mwanaharakati wa Habari mwenye umri wa miaka 14 ameuawa akiwa katika jitihada za kutangaza habari za mapigano kati ya vikosi vya kijeshi vinavyoiunga mkono serikali na vile vya waasi katika eneo la Daraa al-Ballad kusini mwa Sryria karibu na mpaka wa Jordan.
Je, Baada ya miaka 50, Chama Tawala cha Malaysia Kitashinda Uchaguzi?
Malaysia wnaajiandaa kwa uchaguzi mkuu wa 13 utakaofanyika Mei 5. Maudhui yanayotawala duru za kampeni za uchaguzi huo ni matarajio makubwa waliyonayo wananchi, au 'ubah' kwa lugha ya wenyeji. Je Chama tawala cha Barisan Nasional, kilichokaa madarakani kwa miaka 50, kitaendelea kutawala nchi hiyo?
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia
Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.