Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Novemba, 2009
Naijeria: Ken Saro-Wiwa Akumbukwa
Chidi Opara anamkumbuka Ken Saro-Wiwa, Mwandishi wa Kinaijeria, mwanaharakati wa mazingira na haki za walio wachache ambaye aliuwawa na watawala wa kijeshi wa Naijeria tarehe 10 Novemba, 1995.
Kenya: Mwai Kibaki na Odinga Budi Washirikiane na ICC
Ubia wa Kuleta Mabadiliko umetoa tamko linalowataka mwai kibaki na raila odinga kushirikiana na mahakama ya kimataifa ya Jinai na kuhakikisha muswada wa Tume Maalum unapitishwa nchini kenya na kurasimishwa kama sheria ndani ya wiki mbili.
Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika (es) kuhusu tukio hilo...
Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa...
Ghana: Vionjo Sehemu ya Kwanza
Sehemu ya kwanza ya vionjo vya Ghana iliyotayarishwa na Gayle: Nchini Ghana, kila kanda ina kitu cha kutoa. Utamaduni, historia, pwani, wanyama na mimea, unaweza ukavivinjari nchini kote, kutokea kwenye mitisitu ya kitropiki kule kusini mpaka mbuga za savana za kaskazini. kama ni mpenzi wa pwani au historia, utaburudika na...
Tunisia: Mwanablogu Fatma Arabicca Awekwa Kizuizini
Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye hublogu kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye Facebook kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri wa miaka 34, ambaye pia anatuhumiwa kublogu kwenye Debat Tunise (Mdahalo wa Tunisia).
Vietnam: Matangazo Mengi Katika Uwanja wa Ndege
Charvey amebaini matangazo mengi kuliko kawaida katika uwanja wa ndege wa Vietnam.
Afrika: Chungu cha Kuiyeyusha Afrika
Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la...
Kenya: Ramani Mpya Ya Wazi ya Kitongoji Cha Kibera Kwenye Blogu
Mradi wenye lengo la kutengeneza ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi, Kenya: “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama vile Ushahidi, UNICEF, Umande Trust na World Bike, walipoonyeshwa mbinu za kutengeneza...
Iran: Majeshi Ya Usalama Yawashambulia Waandamanaji
Kwa mujibu wa Kian majeshi ya usalama yaliwashambulia waandamanaji katika viwanja vya hafteh tir mjini Teheran na kuwajeruhi watu kadhaa.