Habari kutoka na

Wanawake Wanaovaa Nusu Uchi Wataiokoa Sekta ya Utalii Kenya?

  16 Juni 2015

Je, kutembea uchi yanaweza kuwa mbinu bora ya kufufua sekta ya utalii nchini Kenya kufuatia mashambulizi ya wanamgambo wa Al Shabaab?: Seneta mteule, Mbura anasemekana kuwaomba wanawake katika mkoa wa pwani kutembea nusu uchi ili kuwavutia watalii zaidi kuzuru eneo hilo. Wito huo umeibua maswali kuhusiana na thamani ya mwanamke...

Baada ya Maandamano Burkina Faso na Burundi, Naija na Togo Zinafuata?

  8 Juni 2015

Wanaija 20,000 wameingia mitaani mjini Niamey, Naija mnamo Juni, 6. Kuna ababu nyingi za maandamano hayo: umaskini uliokithiri, utawala mbovu na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza yakiwa ni moja wapo ya malalamiko ya asasi za kiraia nchini humo. Maandamano kama haya yalitokea katika nchi za Burkina Faso, Burundi na Togo....

Kuhusu Uamuzi wa Mahakama wa Haki ya Kusaidiwa Kufa Nchini Afrika Kusini

  4 Juni 2015

Profesa Pierre de Vos anaingia rasmi kwenye mjadala mkali kuhusu uwezekano wa kumsaidia mtu kufa nchini Afrika Kusini baada ya Mahakama Kuu nchini humo kuamua kwamba mtu anayekufa ana haki ya kusaidiwa kufa na daktari ili aweze kuyahitimisha maisha yake: Ni muhimu kuona kwamba hukumu hii haimlazimishi mtu kuyakatisha maisha...

Lugha za Pili Zinazoongozwa Kuzungumzwa Zaidi Afrika

  30 Mei 2015

Don Osborne anajadili habari iliyowekwa kwenye tovuti ya Chuo Kikuu cha Olivet Nazarene ikionesha ramani ya “Lugha za pili kuzungumzwa zaidi duniani.” Anaeleza matatizo makuu kutokana na habari hiyo: Suala la kwanza ni kudhani kwamba “lugha inayozungumzwa zaidi kwenye nchi yoyote huwa wazi; mara nyingi, ni lugha ya taifa husika.”...

Tunayoyajua na Tusiyoyajua Baada ya Jaribio la Mapinduzi Nchini Burundi

  20 Mei 2015

Celebration and jubilation near Presidential offices in Bujumbura after the overthrow of Nkurunziza. #BurundiCoup pic.twitter.com/WhJzXKfS69 — Robert ALAI (@RobertAlai) May 13, 2015 Shangwe na vifijo karibu na ikulu ya Rais nchini Bujumbura baada ya kupinduliwa kwa Nkurunzisa. Kufuatia nia ya kugombea urais kwa kipindi cha tatu ya Rais wa Burundi...

Filamu ya Malawi Yawasaidia Wakulima Kujikinga na Mabadiliko ya Tabia Nchi

  24 Aprili 2015

Filamu ya “Mbeu Yosintha” ilitengenezwa kuwasaidia wakulima na wanavijiji kujikinga na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi, hususani kubadilika kwa majira ya mvua kwenye ukanda wa Afrika Kusini Mashariki. Filamu hiyo ni tamthlia inayowatumia wasanii wa ndani ya nchi hiyo na iliandaliwa na mwandishi wa Kimalawi Jonathan Mbuna baada ya...

Mpigania Amani wa Uganda awa Miongoni mwa Watakaoshindania Tuzo ya Amani ya Nobeli

  16 Aprili 2015

This is Uganda (ThisIs256) ni jukwaa la waandishi waliobobea kutoka Uganda walio na utayari wa kuandika habari makini za kuihusu nchi yao, wakilenga kutokomeza uanahabari uchwara, njaa, Ebola, ukabila, pamoja na mambo mengine. Wanachojaribu kukifanya ni kuanzisha aina ya utafiti kuihusu Uganda ambao ni halisi, makini, wa kweli na usio...

Upigaji Kura Unaendelea Tuzo za Blogu Nchini Kenya 2015

  15 Aprili 2015

Sehemu ya kupiga kura kwenye Tuzo za Blogu Nchini Kenya inaendelea mpaka Aprili 30, 2015: Tuzo za Blogu Nchini Kenya hutafuta kuwatuza wanablogu wanaoandika mara kwa mara, wanaoandika madhui yanayosaidia, na wenye ubunifu na ugunduzi. Tuzo hizi ni jitihada za Chama cha Wanablogu Kenya (BAKE) katika kukuza ubora wa maudhui...

Jiandae kwa Mkutano wa MozFest Afrika Mashariki 2015

  1 Aprili 2015

MozFestEA ni tukio litakalofanyika kuanzia Julai 17 – 19, 2015 kwenye Chuo Kikuu cha Victoria, Kampala, Uganda likiwa na maudhui makuu, “Kutafuta Majibu ya Changamoto za Afrika, kwa pamoja mtandaoni”: MozFest Afrika Mashariki ni tukio la kila mwaka linalowaleta pamoja wataalam wa elmu, wabunifu, wasomi na mafundi wa Afrika Mashariki...