Habari kuhusu Picha kutoka Agosti, 2012
Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu
Mvua kubwa ilisababisha mafuriko katika vitongoji vingi ya jiji la Manila pamoja na majimbo ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Mhariri wa Global Voices aliye huko Manila, Mong Palatino, anakusanya picha kutoka katika majukwaa mbalimbali ya habari za kiraia yanayoonyesha athari kubwa ya mafuriko hayo katika mji huo mkuu wa nchi.
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’
Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu
Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.