Habari kuhusu Picha kutoka Aprili, 2012
Senegali:Rais Wade Aandamwa Hata Baada ya Kukubali Kushindwa Uchaguzi
Wakati nchi nyingine zikionekana kushangilia "uungwana" wa Bbdoulaye Wade kukubali matokeo nchini Senegali, wanablogu wa nchi hiyo bado wamemkaba koo Wade kwa kuushambulia Urais wake wakikumbushana ghasia za kuelekea uchaguzi, kubinywa kwa uhuru wa habari na mifano mingi ya utawala mbovu.
Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo
Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.
Indonesia: Maandamano ya Kupinga Bei ya Mafuta Yatikisha Majiji
Miji kadhaa ya nchini Indonesia iligubikwa na maandamano na vurugu za kupinga ongezeko la bei ya mafuta ya petroli katika wiki chache zilizopita. Wanahabari za mtandaoni walijadiliana ikiwa ongezeko hilo la bei lilikuwa jambo sahihi. Watumiaji wa Twita waliongeza nguvu ya wavuti wa kublogu ili kurusha taarifa za mapambano kati ya polisi na wanafunzi jijini Jakarta.
Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje
Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.
Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia
Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.
Taiwan: Kufukuzwa kwenye nyumba kwa nguvu kwa familia kwaitia dosari Sheria ya Ufufuaji Miji
Kufukuzwa kwa kinyama kwa familia ya Wang kulikotekelezwa na serikali ya Jiji la Taipei kulionyesha jinsi haki za raia zilivyo dhaifu mbele ya miradi ya ufufuaji mji. Kumekuwepo na maoni mengi yanayotaka Sheria ya Ufufuaji Miji irekebishwe.
Mexico: Mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwa “Kundi la Harakati kwa ajili ya Amani, Haki na Utu”
Raia wa Mexico wanatoa maoni kuhusu kumbukumbu za mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwa “Kundi la Harakati kwa ajili ya Amani, Haki, na Utu,” ambalo linahusiana na kifo cha mtoto wa mwanaharakati na mtunzi wa mashairi wa zamani Javier Sicilia wakati wa "vita" ambavyo utawala wa sasa umetangaza dhidi ya uhalifu wa kimtandao na kiimla.