· Januari, 2010

Habari kuhusu Picha kutoka Januari, 2010

Baada Ya Tetemeko la Ardhi, Jumbe za Twita Kutoka kwa Walioshuhudia

  14 Januari 2010

Kutokana na janga la tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 ambalo limekikumba kisiwa cha Haiti jioni ya leo (Januari 12), “Haiti” ni mada kuu hivi sasa kwenye huduma ya Twita. Miongoni mwa lundo la jumbe zinazotumwa tena na tena za taarifa za habari kutoka za vyombo vya habari vikubwa na jumbe nyingine za twita zinazotuma sala au dua pamoja na salamu za heri kwa kisiwa hiki cha Karibea, pia kumekuwepo taarifa za mashahidi waliopo kwenye tukio kama vile mwanamuziki na mwendesha hoteli Richard Morse, ambaye anatwiti kwa jina la @RAMHaiti.