· Machi, 2012

Habari kuhusu Wanawake na Jinsia kutoka Machi, 2012

Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu

Kuna masimulizi kusisimua katika siku za hivi karibuni kwenye tovuti ya Global Voices Video za Utetezi ikiwa ni pamoja na haki za wananchi wenyeji na habari za hivi karibuni kutoka Amerika ya Kusini, Mashariki ya Mbali, Ulaya Magharibi na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara zilizochaguliwa na Juliana Rincón Parra.

Korea Kusini: Wahudumu wa ndege wapigania haki ya kuvaa suruali

  25 Machi 2012

Katika Siku ya Wanawake Duniani, wahudumu wa moja ya mashirika makubwa ya ndege nchini Korea Kusini, waliitisha mkutano na waandishi wa habari mbele ya makao makuu ya shirika lao la ndege kudai haki ya kuvaa suruali. Madai hayo yamepata uungwaji mkono mkubwa sana na watumiaji wa mtandao wa nchini humo.

Amerika Kusini: Waathirika wa ‘biashara’ ya kukuza matiti waingia mtandaoni

  24 Machi 2012

Wanawake wengi wameungana kwenye tovuti za kijamii kusema wanachofikiri na kubadilishana taarifa kuhusu matatizo yanayosababishwa na viini vya kukuzia matiti. Wakati huohuo wanapanga hatua gani za kisheria wachukue. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ugonjwa wa saratani huko Amerika ya Kusini. Je, ni kina nani hawa wanaopaaza sauti zao barani humo? Fuatilia ...