Habari kuhusu Teknolojia kutoka Disemba, 2009
China na Iran: #CN4Iran
Jana, maelfu ya Wa-Irani waliingia mitaani ili kupinga dhidi ya utawala wa kiimla. Maandamano hayo yaliwakumbusha watu wa China juu ya vuguvugu la demokrasi la Tiananmen la 1989 na watumiaji...
Israel: Kublogu Kwa Ajili Ya Mazingira Nchini Jordan
“Wanamazingira na Waandishi kutoka Palestina, Jordan na Israel watakutana huko Madaba, Jordan mwezi huu kwa ajili ya warsha ya siku 2: “Kublogu kwa Ajili ya Mazingira” tarehe 20-21 Desemba,” anaandika...
Poland: Blogu Zataka Malipo
Wasomaji wa blogu zinayoongoza za lugha ya Kipolish ni lazima wameshangazwa kuona kivinjari skrini mpya ya ukaribisho kwenye moja ya tovuti zinazopendwa: Imetangaza kwamba, kuanzia Disemba 14, 2009, kupatikana kwa blogu hiyo hakuta kuwa bila ya gharama. Jakub Gornicki anaandika kuhusu habari hiyo.
Namibia: Nafasi ya Vyombo Vipya vya Habari kwa Uchaguzi wa 2009
Uchaguzi wa rais na bunge la taifa la Namibia ulifanyika tarehe 27 na 28 Novemba 2009. Vyama vya siasa na mashirika yasiyo ya kiserikali yalitumia nyenzo kadhaa za habari za kijamii kupiga kampeni, kufuatilia na kuripoti Uchaguzi.
Twita Kutoka Beirut: Siku ya Pili ya Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni
Siku ya pili ya Warsha ya Wanablogu wa Kiarabu ilianza na mada inayohusu Mtandao wa Herdict, tovuti inayotumia vyanzo vya watumiaji kukusanya taarifa za uchujaji wa habari kwenye intaneti kutoka...
Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni: Tafakuri ya Twita kwa Siku ya Kwanza
Wakati siku ya kwanza ya Warsha ya Pili ya Mwaka ya Wanablogu wa Uarabuni ikifungwa, tutaangalia tafakuri za washiriki kwa siku nzima, kujua wamejifunza nini na namna wanavyojisikia. Siku ilianza...
Indonesia: Sarafu za Kudai Haki
Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.
Nyenzo ya Mtandaoni ya Kufuatilia Mabadiliko ya Tabianchi
Kuelekea kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya TabiaNchi utakaofanyika Copenhagen (COP15) mwezi Desemba 2009, zifuatazo ni baadhi ya nyenzo za mtandoni za kufuatilia mabadiliko ya Tabia Nchi.
Urusi: Jinsi Abiria wa “Nevsky Express” Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii
Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?