· Juni, 2013

Habari kuhusu Maandamano kutoka Juni, 2013

Mtu Mmoja Afariki Kwenye Maandamano Yanayoitikisa Brazil

  28 Juni 2013

Kijana mdogo aliuawa baada ya kugongwa na gari huko Ribeirao Preto na dazeni ya watu wengine walijeruhiwa pale waandamanaji walipokuwa wakikabiliana na polisi katika majiji ya Brasilia, Rio de Janeiro na Salvador kufuatia watu zaidi ya milioni moja kujitokeza katika mitaa ya majiji makubwa na madogo nchini kote Brazil katika maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kushuhudiwa nchini humo kwa miongo miwili.

PICHA: Mamia Wakamatwa Nchini Brazil kwa Kupinga Ongezeko la Nauli za Mabasi

  22 Juni 2013

Polisi wanakabiliana kwa vurugu na kwa kutumia moshi wa machozi dhidi ya waandamanaji wanaopinga ongezeko la nauli ya usafiri wa umma katika maandamano ya yalioyodumu kwa siku ya nne mfululizo huko Sao Paulo. Maandamano haya ni sehemu ya Harakati za Kudai Usafiri wa Bure ambazo tayari zimeshasambaa katika miji mikuu mingine yote nchini Brazil.

Kukamatwa kwa Mwandishi wa Habari wa Kimasedonia Kwachochea Maandamano

Waandishi wa habari wa Kimasedonia walikusanyika [tazama video na soma nakala] mbele ya Mahakama ya Makosa ya Jinai hivi leo katika mji mkuu Skopje kupinga kukamatwa kwa mwenzao, Tomislav Kezarovski, kwa mujibu wa maandishi haya [en] yaliyoandikwa katika ukurasa wa kundi la Kimasedonia kwenye mtandao wa Facebook yaliyopewa kichwa cha habari cha “Waandishi wa...

Ukatili wa Polisi Nchini Macedonia: Miaka Miwili Baadae

Siku ya Alhamisi, Juni 6, katika kituo cha Skopje, Vuguvugu la Kupinga Ukatili wa Polisi litatimiza miaka miwili baada ya mauaji ya Martin Neshkovski, ambayo yalisababisha maandamano makubwa katika ngazi za chini kabisa nchini Macedonia katika majira ya joto ya 2011. Tukio la Facebook [mk] kuhusu ibada ya kumbukumbu linaeleza: Siku ya Alhamisi,...

Wafanyakazi wa Sekta ya Afya Nchini Msumbiji Wagoma Kudai Maslahi

Wafanyakazi wa sekta ya afya nchini Msumbiji wamekuwa katika mgomo uliodumu kwa siku kumi na kusababisha kusimama kwa huduma katika vitengo vingi vya kutoa huduma za afya kote nchini humo. Mgogoro wao na serikali umetokana na madai yao ya kuboreshewa maslahi na mazingira ya kazi pamoja na kurekebishwa kwa gharama za chumba cha wagonjwa mahututi katika mahospitali yote nchini humo.