· Aprili, 2012

Habari kuhusu Maandamano kutoka Aprili, 2012

Tunisia: Miitikio Tofauti Kufuatia Kuingiliwa kwa Barua Pepe za Waziri Mkuu

Mnamo Aprili 8 “Anonymous Tunisia” kikundi kisichotambulisha majina ya wanachama wao nchini Tunisia (ambacho kinadai kuwa na uhusiano na kikundi cha watu “wasiojitambulisha” ) waingiliao mawasiliano ya watu kiliingilia mawasiliano the ya barua pepe ya waziri mkuu wa Tunisia Hamadi Jebali. Vuguvugu hilo lilipewa jina la utani la (“Achana na Tunisia yangu”) ambayo ni sehemu ya kampeni kuu iitwayo “Operesheni Rejeza Tunisia”.

30 Aprili 2012

Indonesia: Maandamano ya Kupinga Bei ya Mafuta Yatikisha Majiji

Miji kadhaa ya nchini Indonesia iligubikwa na maandamano na vurugu za kupinga ongezeko la bei ya mafuta ya petroli katika wiki chache zilizopita. Wanahabari za mtandaoni walijadiliana ikiwa ongezeko hilo la bei lilikuwa jambo sahihi. Watumiaji wa Twita waliongeza nguvu ya wavuti wa kublogu ili kurusha taarifa za mapambano kati ya polisi na wanafunzi jijini Jakarta.

15 Aprili 2012

Mexico: Mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwa “Kundi la Harakati kwa ajili ya Amani, Haki na Utu”

Raia wa Mexico wanatoa maoni kuhusu kumbukumbu za mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwa “Kundi la Harakati kwa ajili ya Amani, Haki, na Utu,” ambalo linahusiana na kifo cha mtoto wa mwanaharakati na mtunzi wa mashairi wa zamani Javier Sicilia wakati wa "vita" ambavyo utawala wa sasa umetangaza dhidi ya uhalifu wa kimtandao na kiimla.

1 Aprili 2012