Habari kuhusu Maandamano kutoka Aprili, 2010
Irani: Je Blogu Zimepoteza Umaarufu Tangu Uchaguzi
Je uchaguzi wa rais ulibadili jinsi nyenzo za uanahabari wa kiraia zinavyofanya kazi nchini Irani? Wanablog wa Irani kumi na moja na wandishi wa habari wanaowakilisha sehemu tofauti za misimamo ya kisiasa wamejibu dodoso kuhusu mabadiliko uanahabari wa kiraia nchini Irani tangu Uchaguzi.
Guatemala: Hadithi ya Maziwa Mawili, Macaws na Malkia
Wanaharakati wa mazingira wana hofu kuhusu kuendelea kuchimbwa mafuta katika Hifadhi ya taifa ya Laguna del Tigre, ambayo ni moja ya maziwa ya asili nchini guatemala ambalo lina utafuti wa mazingira na ambalo liko hatarini.
Poland: Utata Kuhusu Sehemu Atakayozikwa Rais wa Poland
Tangazo la leo kuwa rais wa Poland na mke wake, waliofariki katika ajali mbaya ya ndege huko Smolensk Jumamosi iliyopita, watazikwa katika Kasri la Wawel huko Krakow limezua utata mwingi. Sylwia Presley anatafsiri mitazamo ya baadhi ya wanachama wa Facebook wa kiPoland.
Kirigistani: Mapinduzi “Yaliyowekwa kwenye Kumbukumbu”

Mnamo tarehe 6 April, nchi ya Kirigistani ilikumbwa na maandamano makubwa ya kupinga utawala ambayo hatimaye yaliing'oa serikali pamoja na kusababisha vifo vya watu wengi. Pamoja na kwamba intaneti haikushika usukani katika kuhamasisha maandamano hayo, imetumika sana katika kuhifadhi kumbukumbu za kina za maandamano hayo.
Indonesia: Sony yamkabili Sony
Sony AK wa Indonesia alitishiwa kushitakiwa kwa kukiuka sheria za matumiza ya nembo na shirika la Sony la Japan kama hatafunga tovuti yake binafsi yenye jina www.sony-ak.com. Suala hili lilizua mwitiko mkali katika jamii ya wanamtandao na kuilazimisha kampuni ya Sony kutupilia mbali shauri hilo.