Habari kuhusu Siasa kutoka Machi, 2014
“Iran haiwezi kuufungia Mtandao wa Facebook Milele”
Waziri wa Utamaduni na Ulinzi wa Uislamu wa Iran, Ali Jannati, alisema “Iran haiwezi kuufungia Mtandao wa Facebook milele.” Maofisa kadhaa wa Iran kama Mohammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Kigeni, hutumia mitandao ya Twita na Facebook hata wakati tovuti hizo zimefungiwa nchini Iran.
Iran: Mwanafunzi Ahukumiwa Miaka 7 Jela
Blogu ya PersianBanoo iliripoti kuwa “mwanafunzi mwanaharakati wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Qazvin aliyefukuzwa, Maryam Shafipour amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela. Awali iliripotiwa na familia yake kuwa alikuwa amepigwa na maofisa wa kiume waliokuwa wanamhoji wakati wa kuhojiwa kukiendelea”.
Aliyoyaandika Waziri Mkuu wa Urusi Medvedev Kwenye Mtandao wa Facebook Kuhusu Ukraine
Waziri Mkuu wa Urusi Medvedev amechagua eneo lisilotarajiwa kusemea tamko lake kuhusu Yanukovich na namna anavyoiona hali ya uongozi wa kisiasa iliyopo Ukraine.
Trinidad na Tobago: Kati ya Serikali Mbili
Katika mukhtadha wa idadi na ukubwa wa miradi inayotekelezwa kwa kupitia mipango ya serikali ya nchi hiyo, Afra Raymond anaeleza kwa nini ushirika wa kiwango cha juu unaoonyeshwa hivi sasa na Trinidad na Tobago kwa China ni “suala nyeti linalostahili tafakuri ya kina.”