Habari kuhusu Habari za wenyeji
Chile: Mahabusu wa Mapuche Wamaliza Mgomo wa Kutokula Uliodumu kwa Siku 60
Baada ya siku 60 za mgomo wa kutokula, mahabusu wanne wa Mapuche wamesitisha mgomo wao mara baada ya Mahakama Kuu ya Chile kukubaliana na baadhi ya madai yao. Juhudi hizi pia zimepelekea kuwepo kwa migowanyiko kiasi kuhusiana na mgogoro miongoni mwa watu wa Chile.
Guatemala: Waandamanaji Wazawa 7 Wauawa Totonicapán
Raia wasiopungua 7 wameuawa, takribani watu 32 wamejeruhiwa na 35 walidhuriwa na sumu mnamo tarehe 4, Oktoba, 2012 wakati majeshi ya muungano yalipotumia nguvu kuwatawanya waandamanaji kutoka katika njia panda maarufu inayoeleka jiji la Guatemala City.
Paraguai: Kutoka Kutumikishwa Hadi Kuwa Kiongozi Mzawa.
Kutana na Margarita Mbywangi, ambaye katika umri wa miaka mitano, alichukuliwa kutoka kwa wazazi wake na kuuzwa mara kadhaa na kulazimishwa kufanya kazi za nyumbani. Tangu wakati huo amekuwa kiongozi muhimu wa kabila la Aché na hata kuwa Waziri katika nchi yake. Mbywangi sasa anasimulia maisha yake binafsi kupitia Mradi wa Rising Voices.
Ajentina: Dokumentari Kuhusu Wenyeji wa Mjini Yatafuta Tafsiri ya Maandishi
Dokumentari iitwayo Runa Kuti iliyoshirikishwa katika mradi wa Haki miliki wa “Creative Commons” kuhusu kutambuliwa kwa wananchi waliotokana na uzao wa wenyeji wa zamani walioishi mjini katika jiji la Buenos Aires, inatafuta watu wa kujitolea kusaidia kuiwekea video hiyo tafsiri ya maandishi kwenda katika lugha za asili za Ajentina kama ki-Quechua, ki-Aymara, -kiMapuche na ki-Guaraní pamoja na ki-Kiingereza.
Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu
Kuna masimulizi kusisimua katika siku za hivi karibuni kwenye tovuti ya Global Voices Video za Utetezi ikiwa ni pamoja na haki za wananchi wenyeji na habari za hivi karibuni kutoka Amerika ya Kusini, Mashariki ya Mbali, Ulaya Magharibi na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara zilizochaguliwa na Juliana Rincón Parra.
Peru: Kampeni ya Kuzuia Kufungwa kwa Maktaba ya Amazon
Juan Arellano wa Globalizado [es] anaripoti juu ya kampeni ya kuzuia kufungwa kwa maktaba huko Iquitos, Peru , maktaba ambayo inatilia mkazo vitabu na masuala yanayohusu Amazon. Maktaba hiyo ni ya pili kwa umuhimu katika masuala ya Amazon huko Marekani ya Latini.
Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine
Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.
Nyenzo ya Mtandaoni ya Kufuatilia Mabadiliko ya Tabianchi
Kuelekea kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya TabiaNchi utakaofanyika Copenhagen (COP15) mwezi Desemba 2009, zifuatazo ni baadhi ya nyenzo za mtandoni za kufuatilia mabadiliko ya Tabia Nchi.
Paraguay: Wenyeji Wanyunyiziwa Dawa za Kuua Wadudu kwa Ndege
Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.
Trinidad & Tobago: Kampeni ya 350
“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: Attillah Springer anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.