Habari kuhusu Afya
Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini Liberia Wawekwa Shakani Kufuatia Vita Dhidi ya Ebola
Umoja wa wanahabari wa Liberia wasikitishwa na hali ya kukosekana kwa uhuru wa upashanaji habari kufuatia hatua ya serikali ya kuzuia kuenea kwa virusi vya ebola. Umoja huu ulimwandikia barua Waziri wa sheria kumtaka kutafakari upya madhila wanayokabiliana nayo waandishi wa vyombo vya habari. Ufuatao ni muhtasari wa barua yenyewe:...
Maktaba ya Digitali ya Tiba Asilia Nchini Ufilipino
Ikiwa imeanzishwa na mamlaka kadhaa za kiserikali, Maktaba Dijitali ya Elimu ya Tiba za Jadi Ufilipino (TKDL-Health) inalenga kuweka kumbukumbu na kufanya masuala ya tiba za jadi kuwa za kidijitali nchini humo. Jamii, ambazo nyingi ni zile za miliamni au majirani zao, zimekuwa zikitegemea miti na mazao mengine ya asili...
Nzige Wavamia Mji Mkuu wa Madagaska
#valala pic.twitter.com/YHzOx5Q8QU — Vaintche Rahouli (@vincraholi) Agosti 28, 2014 Watumiaji-mtandao wa Twita na Facebook kutoka mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wamepachika picha kadhaa za nzige wakivamia mji. Uvamizi wa nzige sio tukio la ajabu nchini Madagaska, hasa baada ya dhoruba za kitropiki, lakini sio kawaida katika miji mikubwa. Nzige wanaweza...
Baraza la Mawaziri Nchini Zambia Lichunguze Afya ya Rais
Kwa mtazamo wa tetesi zilizoenea sana kuhusu afya ya rais wa Zambia, Michael Sata, Gershom Ndhlovu ana hoja kwamba katiba inalipa Baraza la Mawaziri mamlaka ya kuchunguza afya yake: Mara ya mwisho rais wa Zambia Michael Sata kuonekana hadharani ilikuwa takribani Juni 20 ambapo alikuwa mwenyeji wa ujumbe wa serikali...
Rais wa Zambia Ajaribu Kuthibitisha Kuwa Yuko ‘Fiti’ kwa Picha Hizi za Facebook. Baadhi Hawajashawishika
Raia wa Zambia wanaendelea kuwa na wasiwasi wa safari za kimya kimya anazofanya Rais Sata nje ya nje, ambazo zimekuwa zikiitwa na serikali kuwa likizo za kikazi
Jinsi Mabadiliko ya Hali ya Hewa Yanavyowaathiri Wakaazi wa Vijiji Nchini Benin
Mbenin, Alain TOSSOUNON, alipachika muhtasari wa ripoti kwenye blogu ya Mtandao wa Afrika Magharibi wa Waandishi wa Habari Unaohusu Maji na Usafi wa Mazingira (WASH). Ripoti yenyewe ilishughulikia tathmini ya mahitaji ya baada ya maafa nchini Benin kufuatia mafuriko makubwa ya hivi karibuni. Maafa hayo yalisababisha vifo vya karibu watu...
Rwanda: Mema, Mabaya na Matumaini
Ingawa Rwanda imepiga hatua kubwa katika kuponya majeraha ya mauaji ya kimbari ya 1994, makundi ya utetezi yanaripoti vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu.
“Hatujaweka Mkazo vya Kutosha Kwenye Afya ya Vijana”
Ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu afya ya vijana duniani inabainisha kwamba: Sababu kubwa za vifo vya vijana duniani ni ajali za barabarani, VVU?UKIMWI, na kujiua. Duniani kote, wastani wa vijana milioni 1.3 walipoteza maisha yao mwaka 2012. Ripoti inaongeza vile vile kuwa :...
Kurekebisha Historia: Sauti ya Wahanga Waliolazimishwa Kuwa ‘Wagumba’ Nchini Peru
Likiwa na lengo la kukusanya saini 3,000, shirika la MujeresMundi limeanzisha madai ya mtandaoni kwenye jukwaa la Change.org likiitaka serikali ya Peru kujenga upya kumbukumbu ya kihistoria kwa sauti ya wahanga wa dawa za ugumba: […] kipindi cha pili cha serikali ya Alberto Fujimori; sera ya Taifa ya Afya ya...
Magonjwa ya Afya ya Akili Hayapewi Kipaumbele Nchini Cambodia
Akiandika kwa niaba ya Southeast Asia Globe, Denise Hruby aliripoti jinsi wagonjwa wa akili katika maeneo mengi ya vijijini vya Cambodia wanavyofanyiwa: …Wagonjwa wa akili bado hutibiwa na waganga wa jadi, ambao lengo lao ni kuwatoa pepo wabaya kwa kuchoma ngozi, au kwa wafanyakazi wasio na ujuzi wa chumba kimoja...