Habari kuhusu Chakula
Zambia Yapanga Bei ya Mahindi kwa Mara Nyingine, Yaikasirisha Benki ya Dunia
Kupanda kwa bei ya mahindi, chakula kikuu nchini Zambia kumesababisha raia kufanya ghasia na hata kusababisha jeshi kuingilia kati. Pamoja na tahadhari iliyotolewa na benki ya dunia kwamba hatua hiyo ingeathiri sekta ya kilimo, watawala wa nchi hiyo wameendelea kupanga bei ya unga wa mahindi.
Suluhisho la Kiradikali la Umaskini Duniani: Ufunguzi wa Mipaka
Wataalamu kadhaa wanasema kuwa umaskini uliokithiri hauepukiki. Suluhisho la kiradikali zaidi la kupunguza umaskini kwa haraka duniani kwa wataalamu wengi wa uchumi ni kufungua mipaka kati ya nchi na kuruhusu wafanyakazi kuhamia sehemu ambazo nguvukazi inahitajika zaidi.
Msumbiji: Maputo katika Hali ya Tahadhari Kutokana na Machafuko
Jiji la Maputo lipo kwenye hali ya tahadhari wakati machafuko yakisambaa kutokana na kupanda kwa bei ya mkate, maji na umeme. Wakazi wanataarifu kuwepo kwa vurugu mitaani huku hali ikizidi kuwa mbaya.
Syria: Matembezi Kwenye Uwanja wa Blogu
Juma hili, bila utaratibu maalum, Yazan Badran anafanya matembezi kwenye blogu mbalimbali, na mada anuai katika mchanganyiko wa tofauti kidogo na masoko holela ya Aleppo.
Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati
Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.
Morocco: Kusherehekea Idi katika Sehemu za Mashambani
Wikiendi hii iliyopita, Wamoroko walisherehekea Eid Al-Adha. Wanablogu walioko sehemu za vijijini nchini Moroko wanasimulia simulizi zao kuhusu Eid ya mwaka huu. Kwa kuwa upatikanaji wa intaneti upo sehemu chache n amara nyingi ni wa aghali mno nje miji mikubwa, wengi wanaoblugu kutokea sehemu za mashamba ni Wafanyakazi wa Amani wa Kujitolea (PCVs) na kwa hiyo wako katika nafasi ya kuweza kutoa mitazamo kama wageni kutoka nje… walioko ndani.
Pakistani: Tatizo La Sukari Limeifanya Ramadhani Kuwa Chungu
Upungufu wa sukari pamoja na kupanda kwa bei nchini Pakistani mwaka huu kumewaathiri walaji na kumesitisha ongezeko la matumizi wakati wa mwezi wa ramadhani. Wanablogu wa kipakistani wanaichambua hali hiyo.
Mwangwi wa Sakata la Maziwa China katika Afrika
Nchini China inakadiriwa kuwa watoto 13,000 wameugua tangu sakata la maziwa yasiyofaa kuibuka. Ushawishi na nguvu za China vimeongezeka Afrika, kama ulivyoongezeka uagizwaji wa bidhaa za kila namna, kuanzia viatu vya mazoezi mpaka chakula aina ya tambi. Mabloga hata wale walio mbali kama Kongo au Senegal, wanaguswa na usalama wa bidhaa za kutoka China katika nchi zao, na wanafuatilias habari hiyo (ya maziwa yasiyofaa).