Habari kuhusu Elimu kutoka Disemba, 2009
China: Kujitoa Uhai kwa Msomi Mwingine tena – Kisa cha Yang Yuanyuan
YANG Yuanyuan, binti msomi mwenye miaka 30 aliyekuwa na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Shanghai Maritime, alijinyonga kwenye bafu la nyumbani kwake mnamo Novemba 25 mwaka huu. Siku moja kabla hajachukua uamuzi huo alimwambia mama yake kwamba maarifa hayawezi kubadili majaaliwa. Miaka ya hivi karibuni imeshuhudia ongezeko la...
Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari
Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.
Austria: Jinsi Nyenzo Za Habari Za Kijamii “Zinavyoviwashia Moto Vyuo Vikuu”
Je, ulijua kwamba katika wakati huu vyuo vikuu vingi kote Ulaya vinakaliwa na wanafunzi? Vuguvugu hili lote limeratibiwa kwa kutumia nyenzo za uanahabari wa kijamii katika mtandao.
Video: Vijana duniani kote wajieleza kwa sekunde 60
mradi wa OneMinuteJr unawapa vijana......