Habari kuhusu Harakati za Mtandaoni kutoka Machi, 2014
Mazungumzo ya GV: Kipi Kinafuata Nchini Ukraine?
Kipi kinafuata kwenye vuguvugu la maaandamano ya Ukraine? Maandamano na umwagaji damu ulisababisha kung'oka kwa rais anayetuhumiwa kuwa fisadi. Lakini sasa, wakati Urusi ikijiandaa kijeshi na Crimea ikifikiria kujitenga, yapo maswali mengi yasiyoisha kuhusu mustakabali wa kisiasa nchini Ukraine pamoja na uhusiano wake na Umoja wa Ulaya.
Siku 100 Gerezani Bila Mashitaka: Simulizi la Alaa Abd El Fattah
Mwanablogu mashuhuri wa Kimisri Alaa Abd El Fattah amemaliza siku yake ya 100 jela leo pasipo kufunguliwa mashitaka. Tazama video hii kufahamu kuhusu suala lake na mengine zaidi.
Matukio ya Ghasia Zinazofanywa na Majeshi ya Urusi nchini Ukraine
Blogu maarufu ya “Tafsiri za Maida ilichapisha bandiko la mtandao wa Facebook la Dmitry Tymchuk, Mkuu wa Kituo cha Ukraine cha Stadi za Siasa za Kijeshi, linaloeleza matukio ya ghasia za kimataifa zinazodaiwa kufanyika na “matendo yasiyo ya kawaida” tangu Februari 2014. Tymchuk anaanza uchambuzi huu kwa kusema: Kwa mfano,...
Aliyoyaandika Waziri Mkuu wa Urusi Medvedev Kwenye Mtandao wa Facebook Kuhusu Ukraine
Waziri Mkuu wa Urusi Medvedev amechagua eneo lisilotarajiwa kusemea tamko lake kuhusu Yanukovich na namna anavyoiona hali ya uongozi wa kisiasa iliyopo Ukraine.