· Aprili, 2012

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Aprili, 2012

Indonesia: Maandamano ya Kupinga Bei ya Mafuta Yatikisha Majiji

  15 Aprili 2012

Miji kadhaa ya nchini Indonesia iligubikwa na maandamano na vurugu za kupinga ongezeko la bei ya mafuta ya petroli katika wiki chache zilizopita. Wanahabari za mtandaoni walijadiliana ikiwa ongezeko hilo la bei lilikuwa jambo sahihi. Watumiaji wa Twita waliongeza nguvu ya wavuti wa kublogu ili kurusha taarifa za mapambano kati ya polisi na wanafunzi jijini Jakarta.

Mali: Raia Washtushwa na Mapinduzi ya Kijeshi

Askari walioasi wametangaza kwamba wanatwaa madaraka nchini Mali, baada ya kuwa wameteka nyara kituo cha televisheni ya taifa pamoja na ikulu. Wanadai kwamba serikali ilishindwa kuvipa vikosi vya jeshi la nchi hiyo msaada ili kuwakabili vilivyo wapiganaji wa kabila la Tuareg waliokuwa wakiteka miji ya kaskazini mwa nchi hiyo.

Malawi: Maoni ya Mtandaoni Kuhusu Kifo cha Mutharika

9 Aprili 2012

Victor Kaonga anaangalia maoni ya mtandaoni kufuatia habari za kifo cha Bingu wa Mutharika. Mutharika alikuwa rais wa tatu wa Malawi. Alifariki baada ya mshtuko wa moyo asubuhi ya Alhamisi. Hii ni mara ya kwanza kwa Malawi kumzika rais aliyefariki akiwa madarakani.