Habari kuhusu Kichina
Hong Kong: Raia wasema ‘Hapana’ kwa uchaguzi wa meya usio wa kidemokrasi
Kati ya wajumbe wa Kamati ya Kumchagua Kiongozi Mkuu wa Hong Kong wapatao 1,200, wajumbe 689 walimchagua Leung Chun-ying kuwa meya mpya wa jiji la Hong Kong mnamo tarehe 25 Machi. Matokeo yalipotangazwa, maelfu waliandamana ili kupinga jinsi ambavyo Beijing imekuwa ikiuchezea na mchakato wa uchaguzi.
Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011
Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011
China: Pato la Taifa Linaongezeka, Matumizi Katika Huduma za Jamii je?
Tunaendelea kusikia kuwa uchumi wa China unaendelea kukua; je matumizi ya huduma za jamii yameongezeka? Akiba binafsi zinabaki kwenye benki, anaandika mwanablogu mmoja: kutokea hospitali mpaka shuleni mpaka malipo ya uzeeni, China haiwezi kujilinganisha.
China: Kashfa ya Wizi wa Kitaaluma Uliofanywa na Wang Hui, Mtazamo wa Kimataifa
Kuna kashfa ya wizi wa kitaaluma iliyoibuka mwezi Machi katika duru za kitaaluma za Kichina pale Profesa wa Fasihi wa Chuo Kikuu cha Nanjing, Wang Binbin, alipotuhumu kwamba kazi ya uzamizi ya Wang Hui kuhusu Lu Xun – Kugomea Kukata Tamaa – ina aya kadhaa ambavyo vimenukuliwa moja kwa moja...
China: Nchi Imara, Watu Maskini
Shirika la utangazaji la taifa CCTV liliweka wazi mnamo tarehe 28 Juni kuwa China inatarajia kupata yuani trilioni 8 (sawa na dola trilioni 1.18) katika mapato ya fedha kufikia mwisho wa 2010. Mapato hayo kitaifanya China kuwa nchi ya pili kwa ukubwa wa mapato ya fedha baada ya Marekani. Inaoneka...
China: Uchi Ulio Rasmi
Serikali moja ya mji huko katika Jimbo la Sichuan sasa inaitwa “Serikali ya Kwanza nchini China Iliyo Uchi kabisa” baada ya kuwa maafisa wa mji huo kuweka mishahara na matumizi ya serikali kwenye tovuti. Kutajwa kwa suala la ‘uchi au utupu’ katika machapisho mengi ya Kichina katika siku za karibuni...
China: Yatishiwa na Zuio la Mtandao Lililofanywa na Marekani
Maoni kutoka kwa watengeneza programu wa Kichina kuhusu uamuzi wa SourceForge.net wa kufuata sheria za Marekani na kuzuia watumiaji kutoka nchi kadhaa yanajumisha mapendekezo ya jinsi ya kuuzunguka uamuzi huo wa marekani kwenye wavuti wa dunia.
China: Tangazo la Google Kusahihisha Uvumi Limezua Utabiri Mwingine
Tangazo la hivi karibuni la Google.cn linasema kuwa uvumi kuhusu kujitoa kwake ni uvumi tu. Hata hivyo, utabiri zaidi ulijitokeza, ukiuliza iwapo uamuzi wa Google unalenga kuficha kushindwa kwake kibiashara, au unalenga kutumikia maslahi ya kisiasa.
China na Hong Kong: Walinzi na Wauaji
Bodyguards and Assassins (Walinzi na Wauaji) ni filamu ya kuchangamsha iliyotolewa wakati wa Krismasi huko China, Hong Kong na Taiwan. Ikiwa ni filamu ya kizalendo, awali ilipangwa kutolewa mwezi Oktoba ili kusherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Watu wa China lakini ikacheleshwa mpaka mwisho wa mwaka 2009. Tofauti...
China: Adhabu ya Kifo kwa Akmal, ni Tendo la Kufuta Aibu ya Zamani
Akmal Shaikh, raia wa Uingereza aliyeshtakiwa kwa kuingiza mihadarati kinyume cha sheria nchini China, aliuwawa siku ya Jumanne japokuwa familia yake pamoja na serikali ya Uingereza waliomba adhabu ipunguzwe, wakidai kuwa alikuwa ni mgonjwa wa akili. Mahakama Kuu ya China hata hivyo ilikataa ombi la kuangalia hali ya akili ya...