Mosi Simba

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba

Iran: ‘Marufuku Isiyo Rasmi ya Kutembea’ ya Tehran Wakati wa Mkutano wa NAM

Mkutano wa 16 wa Umoja wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote ulianza mnamo tarehe 26 Agosti, 2012 jijini Tehran huku kukiwa na ulinzi mkali. Umoja huo madhubuti (NAM) unaoundwa na nchi ni mabaki ya mvutano uliokuwepo enzi za Vita Baridi kati ya Mashariki na Magharibi, na umoja huu unachukuliwa na Iran pamoja na mataifa mengine kama jukwaa mbadala kwa ajili ya kuendesha mijadala kuhusu masuala mbalimbali yanaoukabili ulimwengu hivi sasa. Iran inasema inapanga mazungumzo kuhusu mpango wa amani ili kukomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria, lakini hakuna uwakilishi kutoka upande wa waasi ulioalikwa kwa sababu Tehran ni rafiki wa karibu wa utawala wa Rais Bashar Assad wa Syria.

Tanzania: Kufungiwa ‘Mwanahalisi’, uhuru wa habari mashakani?

  30 Julai 2012

Mnamo tarehe 30 Julai, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Msajiri wa Habari ilitangaza kulifungia kwa muda usiojulikana gazeti la Kiswahili linalotoka mara moja kila wiki la 'MwanaHalisi'. Ulimwengu wa habari umepokea taarifa hiyo kwa mshtuko mkubwa. Hivi ndivyo wanaharakati wa mtandaoni wanavyoeleza hisia zao kuhusu tangazo hilo.

Zambia: Maoni na Hisia Tofauti baada ya Mwakilishi Kutolewa kwenye Mashindano ya Big Brother

Kuondolewa kwa mwakilishi wa Zambia, mwanamuziki anayefahamika zaidi kwa jina la Mampi, kutoka katika mashindano yanayoendelea ya Big Brother Africa, kumepokelewa kwa hisia na maoni tofauti miongoni mwa watumiaji wa mtandao. Big Brother Africa: StarGame ni toleo la saba la mfululizo wa mashindano hayo maarufu zaidi barani Afrika yanayoonyesha moja kwa moja kupitia televisheni maisha ya washiriki.

Wanablogu wa Kenya: Je, ungependa kushiriki kwenye Mkutano wa Global Voices kuhusu Vyombo vya Habari vya Kiraia pasipo kulipia?

  22 Mei 2012

Mtandao wa Global Voices unawapa wanablogu sita (6) fursa ya kushiriki pasipo kulipia kwenye Mkutano wake unaohusu Vyombo vya Habari vya Kiraia utakaofanyika jijini Nairobi. Ili uweze kushinda moja ya nafasi hizo, andika makala ya walau maneno 500 au pungufu kidogo kuhusu mada hii: "Jinsi gani vyombo vya habari vya kiraia vinaweza kusaidia kufanya uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 2013 uwe wa amani".

Indonesia: Maandamano ya Kupinga Bei ya Mafuta Yatikisha Majiji

  15 Aprili 2012

Miji kadhaa ya nchini Indonesia iligubikwa na maandamano na vurugu za kupinga ongezeko la bei ya mafuta ya petroli katika wiki chache zilizopita. Wanahabari za mtandaoni walijadiliana ikiwa ongezeko hilo la bei lilikuwa jambo sahihi. Watumiaji wa Twita waliongeza nguvu ya wavuti wa kublogu ili kurusha taarifa za mapambano kati ya polisi na wanafunzi jijini Jakarta.