I am a writer, editor and translator of East African origin, and translate web content between English and Swahili and from French to English.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Rose Kahendi
Ousmane Sow : Mwafrika Mweusi wa Kwanza Kushiriki katika Taasisi ya Kifaransa ya Sanaa
Mchonga sanamu Msenegali, Ousmane Sow, alikaribishwa kwenye Académie des Beaux-Arts de Paris [Taasisi ya Sanaa ya Paris] tarehe 11, mwezi wa Disemba. Africa-top-talents.com inaripoti kwamba: Une belle consécration pour ce sculpteur sénégalais connu pour ses séries de sculptures monumentales consacrées aux ethnies africaines (noubas, peuls, masaï, Zoulou). « Mon élection a d’autant plus de valeur à mes yeux...
Jaribio la Mapinduzi? Mgogoro wa Kikabila? Tafakuri ya Machafuko ya Sudan Kusini
Political strife and 500 civilians already reported dead: what, exactly, is behind the current crisis in the world's newest nation?
Uajemi: Washairi Wawili Watiwa Nguvuni
Washairi Mehdi Mousavi na Fatemeh Ekhtesari wametokomea nchini Uajemi. Kwa mujibu wa taarifa za habari, washairi hao wamewekwa kizuizini tangu mwanzoni wa mwezi Desemba. Zaidi ya watu mia mbili wametia saini hati ya malalamiko mtandaoni na kutoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuchukua hatua kuhusiana na hali za wanaharakati wa...
China: Mashindano ya “Akina Mama Wanaotamanisha”
Sina Weibo, tovuti ya Kichina inayofanana na Twitta, imeandaa mashindano ya “Akina Mama Wanaotamanisha.” Picha za washindani zinaonyesha wazi kwamba wengi wao sio akina mama halisi. Hata hivyo, hizo picha zinatuambia mengi kuhusu uhusiano wa kijinsia nchini China. Soma mengine kwenye tovuti ya Offbeat China.
Misri: Picha 27 kutoka Hala'ib
Mwanablogu Mmisri, Zeinobia, amesambaza onyesho hili la picha kutoka Hala'ib, bandari na mji katika mwambao wa Bahari ya Shamu, kwenye Pembetatu ya Hala'ib, karibu na mpaka wa Sudan: Tazama “yasiyoeleweka” kwenye Storify
Hali ya Uhuru wa Dini Nchini Maldivi
Maldivi ni miongoni mwa nchi za kwanza kwenye orodha ya serikali zinazozuia uhuru wa dini. Ni lazima raia Wamaldivi wawe Waislamu, na hawawezi kufuata dini yoyote isipokuwa Uislamu. Wageni wasio Waislamu hawawezi kupiga kura, kuabudu hadharani, kupata uraia, wala kutumikia umma. Kwa maoni ya Mwanahabari Hilath Rasheed, huenda nchi ya...
“Mimi ni Mchuuzi Mjerumani Mjini Dakar”
Muda mfupi baada ya kuwasili kwangu Senegal, nilikutana na kijana. Alinieleza hamu yake ya kuondoka Senegal katika mkutano wetu wa kwanza. Nilitaka kuelewa yaliyosababisha hamu yake ya kuondoka na hali ya maisha yake ya kila siku ili nipate kufahamu maelezo ya kijamii na ya kiutamaduni ya kutaka kwake kuondoka. Alikuwa...
Ulaya Yamuonya Waziri wa Ufaransa Kuhusu Matamshi Yake Dhidi ya Warumi
Matamshi ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa, Manuel Valls, yalifufua uhasama uliokuwepo kati ya Ufaransa na Warumi.
“Nchi” Nzuri ya Afrika
Katika toleo la wikii hii la Brainstorm, jarida la mtandaoni la Kikenya, Brenda Wambui hulaani masimulizi ya sasa kuhusu Afrika: “Afrika ni nchi”, “Afrika inapaa”, ‘”Mitindo ya Kiafrika.” Huchunguza jinsi Wakenya wanavyoweza kukomboa simulizi lao na kujiainisha kwa kuweka masharti yao wenyewe: Kama wenyeji wa Kenya ama nchi nyingine ile,...
Vyombo vya Habari vya Magharibi na Taswira ya Ellen Sirleaf Johnson
Aaron Leaf anajadili jinsi taswira ya rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, hujengwa na vyombo vya habari kimagharibi kama alama ya mambo yote mazuri. Anasema kwamba hili ndiyo simulizi lililomwezesha Sirleaf kuwa mhimili wa maendeleo ya kimataifa na uwezeshaji wa wanawake.