makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Machi, 2010
Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine
Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.
Iraki: Ni Siku ya Uchaguzi Kwenye Twita
Ni siku ya uchaguzi nchini Iraki na ulimwengu wa Twita umekuwa uking’ong’a na habari mpya mpya tangu mapema asubuhi. Waandishi wa habari na wanahabari wa kijamii walijaribu kutumia Twita ili kutupasha habari kuhusu mambo yanavyotukia nchini humo.
Kenya: Mafuriko Makubwa Yapasua Kingo za Mto Ewaso Nyiro Huko Samburu
Alfajiri siku ya Alhamisi, tarehe 4 Machi 2010, mafuriko makubwa yaliikumba Samburu huko kaskazini mwa Kenya na kuharibu nyumba 6 za kulala watalii watalii, baadhi ya kambi za utafiti wa wanyama pori na kuwaacha maelfu wakiwa katika paa za nyumba na kwenye miti. Wimbi hili la maji ya mafuriko lilikuja...
Video: Tetemeko la Ardhi Chile Kwa Kupitia Macho ya Raia
Wakati siku inakaribia kuisha, video zaidi za tetemeko la ukubwa wa 8.8 ambalo liliikumba Chile majira ya saa 9.30 usiku zinajitokeza. Tetemeko hilo, ambalo halikuathiri maeneo ya bara pekee kwa njia ya kusogea sogea kwa ardhi, kadhalika lilisababisha mawimbi ya tsunami mabyo yalizua tahadhari katika eneo zima la Pasifiki huku mataifa mbalimbali yakijiandaa kwa mawimbi hayo pindi yatakapofika kwenye fukwe zao.