Albert Kissima · Julai, 2013

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Albert Kissima kutoka Julai, 2013

Barua ya Wazi ya Kushinikiza Kuachiwa Huru kwa Mwanasheria

  24 Julai 2013

Mnamo Julai 23, 2013, zaidi ya raia 400 wa China wamesaini barua ya kushinikiza serikali ya China kumuachia huru Xu Zhiyong, ambaye ni mwanasheria mashuhuri na mpigania haki aliyekamatwa mnamo Julai 16 baada ya kushinikiza kuachiwa kwa wanaharakati pamoja na kuratibu kampeni dhidi ya uovu unaofanywa na serikali. MRADI WA...

Mwana-Habari Menna Alaa Ashambuliwa na Wafuasi wa Morsi

Mwanablogu na mwanahabari wa video Menna Alaa leo hii ameshambuliwa na waandamanaji wenye hasira wanaomwunga mkono Morsi. Mwanablogu huyo ameweka ushuhuda wake kwa lugha ya kiingereza kwenye makala hii iliyo katika blogu inayokusanya matukio nchini Misri iitwayo Egyptian Chronicles. Anaandika: Kofi nililopigwa usoni, alama iliyobaki usoni mwangu pamoja na kuibwa...

Shindano la Wanablogu wa Kiafrika wenye Fikra Pevu.

Mtandao wa Africa Brains watangaza Shindano la Wanablogu wa Kiafrika Wenye Fikra Pevu watakaowania kitita cha dola Hamsini ($50). Ni muda muafaka wa kutangaza mada ya kwanza, ambayo ni “Teknolojia imekuwa na ushawishi gani katika elimu yako?” Tufahamishe hali ya upatikanaji wa teknolojia ulipokuwa shuleni au chuoni? Tangu uanze kutumia...

India: Chakula Chenye Sumu Chaua Watoto 24

  18 Julai 2013

Chakula kilichoua wanafunnzi na kuwaacha wengine katika hali mbaya kinasadikiwa kuwa kilichanganyikana na dawa ya kuulia wadudu. Tukio hili linaibua maswali kuhusiana na ubora wa chakula cha mchana wanachopewa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini.

Maandamano Yasitisha Ujenzi wa Mtambo wa Nyuklia Kusini mwa China

  16 Julai 2013

Kufuatia siku tatu mfululizo za maandamano, inaonekana kuwa serikali ya Manispaa ya Heshan katika jiji la Jiangmen imesitisha mpango wake wa ujenzi wa mtambo mkubwa wa nishati ya Nyuklia. Baadhi ya watu wanaamini kuwa ushindi huu ni wa muda mfupi tu. Wana wasiwasi kuwa, mradi huu unaweza kuibukia sehemu nyingine karibu na Delta ya mto Pearl, Kusini mwa China mahali palipo na idadi kubwa sana ya watu.

Kuelekea uchaguzi wa Kambodia: Matumizi ya Mtandao wa Facebook

  12 Julai 2013

Watumiaji wa mtandao wa intaneti nchini Cambodia wanatumia mtandao wa Facebook kwa kiwango kikubwa katika kujadili, kuendesha midahalo na kushirikishana mambo mapya yanayohusu chaguzi za kitaifa zinazotarajiwa kufanyika tarehe 28 Julai, 2013. Wakati huohuo, vyama vya siasa pia vinatumia mtandao huu ulio maarufu zaidi katika kuwashawishi vijana wadogo wanaotarajiwa kupiga kura.