Albert Kissima · Januari, 2013

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Albert Kissima kutoka Januari, 2013

Wafalme Watatu Watembelea New York

  14 Januari 2013

Wafalme watatu walikuja na kuondoka, lakini siyo kabla ya kupita katika jiji la New York ili kusherehekea na mamia ya watoto waliojitokeza kwa ajili ya paredi. Shamra shamra hizi za Noeli, kwa karne nyingi, zimekuwa ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Amerika wenye asili ya Karibeani na Walatini..The Three Kings came and went, but not before passing through New York City to celebrate with hundreds of children that came out for the parade. This Christmas celebration has been a part of the Caribbean and Latin American cultural traditions for numerous centuries.

Mwanaharakati wa Pakistani Khudi Ali Auawa Katika Mlipuko wa Bomu

  14 Januari 2013

Mnamo Januari 10, 2013 katika jiji la Quetta lililopo Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Pakistani, watu 82 walipoteza maisha kwenye milipuko ya mabomu yaliyolenga eneo ambalo kimsingi lenye idadi kubwa ya Waislamu wa Shia jamii ya Hazara. Irfan Khudi Ali, mwanaharakati mashuhuri wa haki za binadamu ambaye bila kuchoka aliweka wazi uonevu wa kikabila unaofanywa kwa waShia wa Hazara nchini Pakistan, alifariki katika shambulio lililofuata. Kifo chake kimechochea watu kumpa heshima kwa juhudi zake kwa kuanzisha tena maandamano kupinga mauaji ya watu wa Shia nchini Pakistani.

Mwaka Mpya na Mienendo ya Zamani Nchini Bahrain

Wakati nchi mbalimbali ulimwenguni kote zikiukaribisha mwaka mpya kwa fataki na shamrashamra, serikali ya Bahraini iliandaa utaratibu wa aina yake kwa waandamanaji nchini humo. kwa bahati, watumiaji wa mtandao wa intaneti walikuwa tayari, kuonesha na kuweka kumbukumbu ya baadhi ya matukio kwa ajili ya kushuhudiwa na sehemu nyingine yote ya ulimwengu.

Bangladeshi: Msichana Mwingine Mzawa Abakwa na Kisha Kuuliwa.

  2 Januari 2013

Kwa mara nyingine msichana mzawa ameuawa nchini Bangladesh baada ya kubakwa kikatili. Mhanga huyo, Khomaching Marma (14) alikuwa mwanafunzi wa darasa la nane. Ubakaji huu wa kikatili uliosababisha mauaji kwa mara nyingine tena umeamsha hasira na ghadhabu nchini kote. Watumiaji wa mtandao pia wanapinga vikali vitendo hivyo.

Kusherehekea Mwaka 2012 na Sauti za Dunia

Kadiri mwaka 2012 unavyofikia tamati, tungependa kutoa shukrani zetu kwa kazi nzuri, ubunifu pamoja na kuonesha kujali mambo mengi katika jumuia ya Sauti za Dunia. Mwaka 2012 umekuwa ni mwaka wa ukuaji wa kasi kabisa na wa mafanikio kwa Sauti za Dunia ( Global Voices). Yafuatayo ni baadhi tu ya mafanikio: