Albert Kissima · Oktoba, 2012

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Albert Kissima kutoka Oktoba, 2012

Misri: Ushauri kwa Waandamanaji wa Kuwait

Wakati watu wa Kuwait walipoanzisha maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kutokea ya kuonesha waziwazi kutokukubaliana na mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yaliyopitishwa chini ya mtawala wa kurithi kufuatia kuvunjwa kwa bunge, watu wa Misri wametumia muda wao mwingi katika Twita wakitoa ushauri kwa watu wa Kuwait kuhusiana na yapi ya kufanya na yapi ya kutokufanya.

27 Oktoba 2012

‘Mazungumzo ya Kitaifa’ Nchini Singapore Yatafanikiwa?

Katika juhudi za kupangilia mustakabali wa Singapore, serikali imezindua “mazungumzo ya kitaifa” yatakayodumu kwa mwaka mmoja ili kukusanya maoni ya watu. Baadhi ya wananchi wameupokea mpango huo kwa mikono miwili lakini pia wapo wengine wanaoupinga wakiuona kama mbinu tu ya kujiweka karibu na wananchi.

27 Oktoba 2012

Kuwait: Ni Maandamano Makubwa Kabisa Kuwahi Kutokea?

Mabomu ya kutoa machozi na maguruneti ya kumfanya mtu kupoteza fahamu yalitumika kutawanya maandamano ya kupinga mabadiliko ya sheria ya uchaguzi nchini Kuwait. Maandamano hayo yaliyofanyika siku ya Jumapili, na kuratibiwa kupitia katika mtandao wa Twita na yaliyowavutia takribani watu 150,000 kati ya watu milioni 3 ambao ndio idadi ya watu wa Kuwait. Taarifa za vyombo vya habari zinaichukulia idadi hii kuwa ni kubwa kabisa katika historia ya Falme za ghuba ndogo.

27 Oktoba 2012

India: Mgogoro wa Mtambo wa Nyuklia wa Kudankulam Waendelea.

Mradi wa Nguvu za Nyuklia mjini Koodankulam katika wilaya ya Tirunelveli iliyo katika Jimbo la kusini la Tamil Nadu nchini India umeanza kufanya kazi mwezi uliopita lakini maandamano ya kuupinga mradi huo umeendelea na kamata kamata inasababisha waandamanaji kuishia jela. Juma hili limeshuhudia maandamano yakienea India yote kwa ushirikiano na watu wanaopinga matumizi ya Mtambo wa Nyuklia.

22 Oktoba 2012

Venezuela: ‘Sura na Sauti’ za Uchaguzi

Kwa kutumia mfululizo wa picha na nukuu, mpiga picha wa Kireno Eduardo Leal anayateka mawazo na hisia za watu wa Venezuela kwa jinsi zinavyoeleza watakuwa wanampigia nani kura kuwa Rais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili ya Oktoba 7.Kwa kutumia mfululizo wa picha na nukuu, mpiga picha wa Kireno Eduardo Leal anayateka mawazo na hisia za watu wa Venezuela kwa jinsi zinavyoeleza watakuwa wanampigia nani kura kuwa Rais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili ya Oktoba 7.

8 Oktoba 2012