I am a Tanzanian, professionally a science Teacher specifically for chemistry and Mathematics. I fluently speak Kiswahili. As a Swahili speaker, its my duty to inform swahili speakers around the Globe with news which are hardly found in other news media but only in Global Voices, “Sauti za Dunia, Ulimwengu unaongea, wasikiliza”.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Albert Kissima kutoka Juni, 2012
Misri: Yatambulisha Kipimio cha Morsi
Baada ya miaka 32 ya Hosni Mubarak, Misri imepata rais mpya Mohamed Morsi, na pia kitumizi cha kufuatilia utendaji pamoja na maendeleo ya kutimiza ahadi kuu 64 alizozitoa rais huyo mteule wakati wa kampeni za uchaguzi nchini humo.
Pakistani: Buriani Mehdi Hassan; Mfano wa kuigwa wa Ghazal.
Mehdi Hassan Khan ambaye maarufu alijulikana kama ‘Mfalme wa Ghazal’alifariki dunia Jumatano tarehe 13, Juni, 2012 baada ya kuugua kwa muda mrefu, katika hospitali jijini Karachi nchini Pakistan. wananchi wa Mtandaoni wanattoa salamu zao za mwisho.
Korea ya Kusini: Mabadiliko ya Sheria kuhusu Uzazi wa Mpango Yaibua Mjadala Mkali
Mamlaka ya Chakula na Dawa ya nchini Korea imetangaza kwamba dawa za kuzuia mimba za dharura zinazofahamika kama 'morning-after pills' zitaanza kupatikana kwa wingi. Hata hivyo, dawa za kuzuia mimba zisizo za dharura zimekuwa dawa za kuandikwa na daktari. Mabadiliko haya ya ghafla kuhusu dawa za kuzuia kuzaliana limeibua mjadala mkubwa mtandaoni.