Juni, 2013

Habari kutoka Juni, 2013

Rais Obama Kuitembelea Tanzania

Rais wa kwanza wa Marekani mwenye asili ya Afrika, Barack Obama anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam kesho alasiri kwa ziara ya kiserikali. Blogu ya Swahili Time imeweka ratiba ya...

30 Juni 2013

Kufilisika kwa Watu nchini Malaysia

iMoney.my wametengeneza mchoro unaoelezea takwimu za kufilisika nchini Malaysia. Wastani wa matukio 20,000 ya kufilisika yamerekodiwa mwaka 2012 hiyo na maana kwamba wa-Malaysia 53 wanafilisika kila siku.

30 Juni 2013

Bahrain: Sheria Mpya za Kudhibiti Huduma ya Skype na Viber

"Tahadhari za Kiusalama" zinatajwa kuwa sababu zilizolazimisha kutungwa kwa sheria mpya zinazoweza kuhitimisha matumizi ya huduma maarufu za Skype, WhatsApp, Viber na Tango nchini Bahrain. Afisa wa serikali alisema utafiti unafanywa kuweza kudhibiti zana tumizi za mawasiliano ya sauti mtandaoni - huduma zinazotumika sana, na zinazosababisha hasara kubwa kwa makampuni ya simu.

30 Juni 2013

Wanaharakati 36 wa Azeri Wakamatwa nchini Iran

Wanaharakati thelathini na sita wa Azeri akiwamo mwanablogu mmoja, Kiaksar, walikamatwa siku ya Alhamisi, 27 Juni katika eneo la Urmia. Vikosi vya usalama viliwaachilia huru wanaharakati hao 300 baada ya...

29 Juni 2013

Mtu Mmoja Afariki Kwenye Maandamano Yanayoitikisa Brazil

Kijana mdogo aliuawa baada ya kugongwa na gari huko Ribeirao Preto na dazeni ya watu wengine walijeruhiwa pale waandamanaji walipokuwa wakikabiliana na polisi katika majiji ya Brasilia, Rio de Janeiro na Salvador kufuatia watu zaidi ya milioni moja kujitokeza katika mitaa ya majiji makubwa na madogo nchini kote Brazil katika maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kushuhudiwa nchini humo kwa miongo miwili.

28 Juni 2013

Uzuri wa Mlima Everesti Nyakati za Usiku

Sinema fupi za Elia Saikaly zimenasa uzuri mkuu wa Mlima Everesti nyakati za usiku kwa kila sekunde. Anasimulia kwenye blogu yake uzoefu wake wa kupanda hadi kilele cha Mlima Everest...

27 Juni 2013

PICHA: Mamia Wakamatwa Nchini Brazil kwa Kupinga Ongezeko la Nauli za Mabasi

Polisi wanakabiliana kwa vurugu na kwa kutumia moshi wa machozi dhidi ya waandamanaji wanaopinga ongezeko la nauli ya usafiri wa umma katika maandamano ya yalioyodumu kwa siku ya nne mfululizo huko Sao Paulo. Maandamano haya ni sehemu ya Harakati za Kudai Usafiri wa Bure ambazo tayari zimeshasambaa katika miji mikuu mingine yote nchini Brazil.

22 Juni 2013

Raia wa Myanmar Wachukizwa na Mashambulizi Dhidi ya Wahamiaji Wenzao Nchini Malasia.

Vurugu za kikabila nchini Mynmar inaonekana kusambaa hata katika nchi za jirani.. Baadhi ya wahamiaji wa Mynmar wa jamii ya budha wanaoishi nchini Malasia wiki chache zilizopita ambapo watu wengi wanaamini kuwa mashambulia hayo yanahusiana mvutano wa kimakabila na kidini unaoendelea nchini Myanmar. Mwitikio wa awali wa serikali ya Myanmar wa kukanusha matukio haya uliwakasirisha watumiaji wengi wa mtandao.

21 Juni 2013

Maandamano ya Kudai Uhuru Yafanyika Kwenye Miji ya Saudi Arabia.

Makundi madogo madogo ya wanawake wa Saudi Arabia kwa wakati mmoja yaliitisha “mikutano ya kudai uhuru” katika maeneo mbalimbali ya majiji ya Saudi Arabia mnamo tarehe 10 Juni, 2013, maandamano yaliyoratibiwa na kundi lisilojulikana la mawakili @almonaseron [ Waungaji mkono] linaloshinikiza kuachiwa huru kwa ndugu zao wanaoshikil

16 Juni 2013