Mei, 2013

Habari kutoka Mei, 2013

Jamhuri ya Dominika: Mwanafunzi Auawa kwenye Maandamano

Mnamo siku ya Alhamisi ya tarehe 8 Novemba, 2012, Chuo Kikuu cha Santo Domingo kiligeuka kuwa uwanja wa maandamano yanayopinga mpango wa serikali kubana matumizi. Wakati wa maandamano, polisi walisababisha kifo cha mwanafunzi wa udaktari mwenye miaka 21, William Florián Ramírez. Haikuchukua muda mrefu sakata hilo lilihamia katika mitandao ya kijamii.

28 Mei 2013

Saudi Arabia Yawanyonga Raia Watano wa Yemeni na Kutundika Miili Yao Hadharani

Raia watano wa Yemeni waliotiwa hatiani kwa mauaji na ujambazi walinyongwa kwa kukatwa kichwa nchini Saudi Arabia na miili yake kuanikwa hadharani huko Jizan, mji ullio kusinimagharibi mwa nchi hiyo. Picha za miili hiyo ikining'inia kwenye kamba hewani ilisambaa kwenye mtandao wa Twita na facebook kama hatua ya wa-Yemeni kupinga ukatili huo.

26 Mei 2013