Habari kutoka Mei, 2013
Lebanon: Mwanablogu Apata Kipigo kwa Kupiga Picha
Mwanablogu wa ki-Lebanoni Habib Battah anaeleza namna alivyoshikiliwa bila hiari, akilazimishwa kufuta picha katika kamera ya simu yake na kudhalilishwa mfululizo katika posti hii inayohusiana na ripoti ya Beirut. Aliporipoti...
Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania
Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris...
Kwa nini Mashirika ya Umma Yameshindwa Nchini Zambia
Elias Munshya, mwanasheria na mchungaji wa Zambia, anaeleza kwa nini mashirika ya umma yamedumaa nchini Zambia tangu uhuru: Mashirika ya umma hayajawahi kutengeneza faida tangu mwaka 1964. Yamekuwa yakiendeshwa kiholela...
Botswana: Kuibwa kwa Kazi ya Sanaa ya “Bushman's Secrets”
MyWeku anaichambua filamu yenye maudhui halisi (documentary) inayoelezea wizi wa kazi ya sanaa ya Sana iitwayo “Bushman's secrets”: Filamu hii inachora picha inayosikitisha ya namna ambavyo Uniliver, kampuni inayojinadi kama...
Jamhuri ya Dominika: Mwanafunzi Auawa kwenye Maandamano
Mnamo siku ya Alhamisi ya tarehe 8 Novemba, 2012, Chuo Kikuu cha Santo Domingo kiligeuka kuwa uwanja wa maandamano yanayopinga mpango wa serikali kubana matumizi. Wakati wa maandamano, polisi walisababisha kifo cha mwanafunzi wa udaktari mwenye miaka 21, William Florián Ramírez. Haikuchukua muda mrefu sakata hilo lilihamia katika mitandao ya kijamii.
Rais wa Chama cha Madaktari Msumbiji Akamatwa
Baada ya mgomo wa madaktari uliodumu kwa takribani juma moja nchini Msumbuji, Dr. Jorge Arroz, Rais wa Associação Médica de Moçambique, amekamatwa usiku wa Jumapili, Mei 26, 2013, kwa tuhuma...
Saudi Arabia Yawanyonga Raia Watano wa Yemeni na Kutundika Miili Yao Hadharani
Raia watano wa Yemeni waliotiwa hatiani kwa mauaji na ujambazi walinyongwa kwa kukatwa kichwa nchini Saudi Arabia na miili yake kuanikwa hadharani huko Jizan, mji ullio kusinimagharibi mwa nchi hiyo. Picha za miili hiyo ikining'inia kwenye kamba hewani ilisambaa kwenye mtandao wa Twita na facebook kama hatua ya wa-Yemeni kupinga ukatili huo.
Rafael Correa Aapishwa kwa Kipindi cha Tatu Kama Rais wa Ekuado
Rafael Correa ameapishwa kuingia ikulu kama Rais wa Jamhuri ya Ekuado kutawala mpaka 2017..
Shambulio la Mabomu Mawili ya Kujitoa Muhanga Nchini Niger Yaua Watu 23
Benjamin Roger wa Jeune Afrique anaripoti [fr] kuwa wanajeshi 18, raia mmoja na magaidi wanne waliuawa mapema subuhi ya leo katika shambulio la mabomu ya kujitoa Muhanga kwenye gari mjini...
‘Igundue Somalia’ Blogu ya Picha na Utamaduni
Igundue Somalia ni blogu ya Picha na Utamaduni maalumu kwa Somalia. Blogu hiyo inakusudia kutangaza vyema sura sahihi ya Somalia kwenye vyombo vya habari na vipaji vya watu wake, masuala...