Disemba, 2012

Habari kutoka Disemba, 2012

Chama cha Upinzani NPP Chapinga Matokeo ya Urais Ghana Mahakamani

Chama Kikuu cha Upinzani nchini Ghana, NPP, kimegoma kuyakubali matokeo ya uchaguzi wa Rais. Mnamo tarehe 9 Desemba 2012, Tume ya Uchaguzi ilimtangaza Rais Mahama kuwa mshindi kwa asilimia 50.70 ya kura, akimshinda mshindani wake wa maribu Nana Akufo-Addo wa NPP. Chama cha NPP hapo awali kilifungua mashitaka katika Mahakama Kuu tarehe 28 Desemba, 2012.

30 Disemba 2012

China Inaelekea Wapi kwa Mwaka 2013?

Kadri mwaka wa 2012 unavyosogea karibu, jarida la CHINA DIGITAL TIMES limetoa muhtasari wa mabadiliko na changamoto zinazoikabili China mwaka 2013 kwa kutumia taarifa na bashiri mbalimbali za vyombo vya...

29 Disemba 2012

Assad atumia Ndege ya Kivita Kuwaua Raia Wake

Serikali ya Syria imefanya shambulizi kubwa la angani dhidi ya raia wa nchi hiyo -waliokuwa wamesimama kwenye foleni waisubiri mikate kwenye kiwanda cha kuokea miakte huko Halfaya, Hama. Inakadiriwa kwamba watu waliouawa katika shambulio hilo mjini humo ni kati ya 90 na 300, waasi wakisema kuwa watu hao walikuwa wamejitenga na vikosi vya Assad. Mtandaoni, wanaharakati wanashangazwa inakuwaje dunia inaendelea kutazama tu maisha ya watu wasio na hatia wakiuawa kwa mamia.

28 Disemba 2012

Maisha Binafsi ya Watawala Wapya wa China

Shirika la Habari la Xinhua lilichapisha[zh] mfululizo wa wasifu wa maisha binafsi ya watawala wa juu China, ikiwa ni pamoja na picha za familia zao, ambazo ni nadra sana katika...

27 Disemba 2012

Kupigia Kura Maajabu Saba ya Dunia barani Afrika

Shindano la kila mwaka limezinduliwa kwa ajili ya watu kupiga kura kuchagua maajabu saba yaliyo bora zaidi barani Afrika. Na tayari upigaji kura umeshaanza. Baadhi ya maajabu ya asili yaliondolewa katika orodha ya mwisho ya kupigiwa kura na hivyo baadhi ya wanablogu waliongeza mapendekezo yao katika blogu zao. Tazama baadhi ya picha hapa:

27 Disemba 2012

Ni Sikukuu ya Kuzaliwa Kristo (Noeli) Mjini Betlehemu

Ni sikukuu ya kuzaliwa Kristo mjini Betlehemu, katika ukanda wa Magharibi, Palestina, mahali alipozaliwa Yesu Kristo. Ni namna gani nzuri ya kusherehekea tukio hili zaidi ya kuwashirikisha picha na maoni mbalimbali ya watumiaji wa mtandao wa intaneti kuhusiana na tukio hili linalosherehekewa na mabilioni ya watu duniani kote.

25 Disemba 2012