Aprili, 2012

Habari kutoka Aprili, 2012

Ajentina: Dokumentari Kuhusu Wenyeji wa Mjini Yatafuta Tafsiri ya Maandishi

Dokumentari iitwayo Runa Kuti iliyoshirikishwa katika mradi wa Haki miliki wa “Creative Commons” kuhusu kutambuliwa kwa wananchi waliotokana na uzao wa wenyeji wa zamani walioishi mjini katika jiji la Buenos Aires, inatafuta watu wa kujitolea kusaidia kuiwekea video hiyo tafsiri ya maandishi kwenda katika lugha za asili za Ajentina kama ki-Quechua, ki-Aymara, -kiMapuche na ki-Guaraní pamoja na ki-Kiingereza.

30 Aprili 2012

Tunisia: Miitikio Tofauti Kufuatia Kuingiliwa kwa Barua Pepe za Waziri Mkuu

Mnamo Aprili 8 “Anonymous Tunisia” kikundi kisichotambulisha majina ya wanachama wao nchini Tunisia (ambacho kinadai kuwa na uhusiano na kikundi cha watu “wasiojitambulisha” ) waingiliao mawasiliano ya watu kiliingilia mawasiliano the ya barua pepe ya waziri mkuu wa Tunisia Hamadi Jebali. Vuguvugu hilo lilipewa jina la utani la (“Achana na Tunisia yangu”) ambayo ni sehemu ya kampeni kuu iitwayo “Operesheni Rejeza Tunisia”.

30 Aprili 2012

Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo

Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.

30 Aprili 2012

Bangladesh: Mahakama Yaamuru Kufungwa kwa Kurasa za Facebook kwa Kukashifu Dini

Mnamo tarehe 21 Machi, mahakama moja huko Bangladesh iliziamuru mamlaka zinazohusika kuzifungia kurasa tano za Facebook na tovuti moja kwa kukashifu Mtume Mohamedi, Kuruani na dini nyinginezo. Wanaharakati wa mtandaoni wana hofu kwamba kama amri hiyo itatekelezwa, basi itafungua milango kwa uhuru wa kujieleza kudhibitiwa katika siku za usoni.

23 Aprili 2012

Ghana: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kiraia katika Uchaguzi wa Mwaka 2012

Wananchi wa Ghana wanajitayarisha kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge ambao utafanyika tarehe 7 Disemba 2012, Jumuiya ya wanablogu wa Ghana imezindua mradi wa uanahabari wa kijamii ambao una nia ya kufunza wanaharakati, vikundi vya kisiasa na wanafunzi kutumia zana za uanahabari wa kijamii kwa ajili ya kwa ajili ya kuafuatilia na kuripoti shughuli za uchaguzi.

16 Aprili 2012

Misri: Kundi la “Muslim Brotherhood” dhidi ya Baraza la Kijeshi – Waonyesha Sura Halisi?

“Maandamano ya watu milioni ya kudai kung'olewa kwa baraza la Ganzouri" ndivyo kilivyosomeka kichwa cha habari cha gazeti rasmi la Freedom and Justice Party kufuatia matukio yaliouacha umma wa Wamisri wakiwa mdomo wazi. Je, nini kimetokea kiasi cha karibia "mvunjiko mbaya" kati ya Baraza la Kijeshi na chama cha kisiasa kilichokuwa karibu kutwaa madaraka, pande ambazo zilikuwa na uhusiano mzuri?

16 Aprili 2012

Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje

Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.

15 Aprili 2012