Aprili, 2010

Habari kutoka Aprili, 2010

Irani: Je Blogu Zimepoteza Umaarufu Tangu Uchaguzi

Je uchaguzi wa rais ulibadili jinsi nyenzo za uanahabari wa kiraia zinavyofanya kazi nchini Irani? Wanablog wa Irani kumi na moja na wandishi wa habari wanaowakilisha sehemu tofauti za misimamo ya kisiasa wamejibu dodoso kuhusu mabadiliko uanahabari wa kiraia nchini Irani tangu Uchaguzi.

24 Aprili 2010

Colombia: Mockus na Fajardo Waungana kwa Ajili ya Uchaguzi wa Rais

Mameya wawili wa zamani wa amajiji 2 makubwa zaidi nchini Kolombia wameunganisha majeshi kugombea katika uchaguzi wa rais wa Mei 30 kwa tiketi moja. Umoja huu mpya wa Chama cha Kijani umepokewa vizuri na watumiaji wa vyombo vya habari vya kijamii, ambo ni sehemu kubwa ya mkakati wa kampeni.

24 Aprili 2010

Piga kura kuchagua “Blogu Bora Zaidi”

Upigaji kura mtandaoni umeanza kwa ajili ya Tuzo ya Blogu Bora Zaidi inayotolewa na Deutsche Welle (Shirika la Habari la Ujerumani), moja kati ya mashindano ya blogu yenye hadhi kubwa kimataifa na blogu zilizotajwa kushiriki ni za lugha kumi na moja tofauti. Unaweza kuipigia kura blogu uipendayo hadi April 14, 2010.

14 Aprili 2010

Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?

Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.

9 Aprili 2010