Habari kutoka Machi, 2010
Serikali ya Japani: Kuhusu Kuanguka kwa Mfumo wa Ajira
Chombo kinachotumika kufanya tafakari nzito cha Baraza la Mawaziri la Japani, Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (内閣府 経済社会総合研究所)(ESRI) kimechapisha matokeo ya utafiti yaliyopima hadhi ya sasa ya ajira...
Jamhuri ya Dominika: Upinzani Dhidi ya Shughuli za Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Barrick
Kumekuwa na ongezeko la upinzani dhidi ya shughuli za Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Barrick kwenye Jamhuri ya Dominika kwa sababu ya vipengele vilivyo kwenye mkataba na manufaa ya dola hilo, vilevile kutokana na sababu mbalimbali za kimazingira.
Global Pulse 2010: Mwaliko wa kuzungumza na watoa uamuzi mtandaoni
Kuanzia tarehe 29 hadi 31 Machi, vuguvugu linalojulikana kama Global Pulse 2010, yaani Mapigo ya Moyo ya Ulimwengu 2010, linakusudia kuwakusanya jumla ya watu 20,000 kupitia mtandao ili wafanya mazungumzo kuhusu mada mbalimbali kuanzia zinazohusu maendeleo ya binadamu hadi sayansi na teknolojia.
Pakistani: Vitendo vya Unyanyasaji Watoto Vyaongezeka
Msemo 'Unyanyasaji watoto' hutumika kueleza vitendo vya aina mbalimbali vilivyo jinai na vinavyofanywa dhidi ya watoto. Wanablogu wanajadili vitendo hivi vya unyanyasiaji watoto vinavyokera na vinavyozidi kuongezeka nchini Pakistani.
Ghana: tamasha la Twestival 2010 Mjini Accra: Shughuli Yenye Maana?
Kama uanahabari wa kijamii unabadilisha mtindo ya mawasiliano katika nchi za Magharibi, basi kwa hakika haujapungukiwa katika kufikia sehemu zinazovutia barani Afrika. . Kwa hiyo haishangazi kwamba MacJordan, wa Global Voices, anashirikiana na Rodney Quarcoo ili kulifikisha tukio hili la kuburudisha kwa watu wa Ghana.
Mali: Vitambaa Vyasuka Nguzo za Uchumi na Utamaduni
Kwa kupitia video, tunaona na kujifunza kuhusu umuhimu wa utamaduni na ongezeko la kiuchumi ambalo utengenezaji vitambaa huwapa baadhi ya watu na mashirika nchini Mali. Vikundi vya wanawake, wasanii na watalii wote wananufaika na utamaduni huu wa kutia rangi vitambaa na upakaji rangi kwa kutumia matope.
Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka
“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa...
Misri: Wafanyakazi wa IslamOnline Wagoma
Mamia ya wafanyakazi, wahariri, na waandishi wa habari walianza mgomo wa kuonyesha hasira yao katika mtandao unaosomwa sana wa jiji la Cairo unaojulikana kwa jina la Islamonline baada ya kuwa wafanyakazi wapatao 250 wamefukuzwa kazi. Kwa mara ya kwanza, wagomaji wanatumia kwa ufanisi na vizuri kabisa aina mpya ya chombo cha habari ili kuvuta usikivu na uungwaji mkono katika kile wanachokipigania, kuanzia na Twita inayoendelea mpaka mmiminiko wa habari wa hapo kwa hapo.
Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema
Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.
Mwaka Mmoja Baada ya Mapinduzi, Viongozi wa Madagaska Wakabiliwa na Vikwazo
Machi 17, 2009 nchini Madagaska, vikwazo vinavyowalenga viongozi wa sasa wa Madagaska vinaandaliwa kwa kushindwa kwao kuheshima makubaliano ya Maputo ambayo hapo awali yalifikiwa na pande zote zinazohusika. Matokeo ya vikwazo hivyo ni pamoja na kuzuiwa kwa mali zinazozalisha fedha na pengine kukamatwa kwa wanaohusika endapo watasafiri nje ya nchi.