- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Mwandishi wa Habari wa Kashmiri Shujaat Bukhari Auawa kwa Kupigwa Risasi

Mada za Habari: Asia ya Kusini, India, Habari za Hivi Punde, Haki za Binadamu, Sheria, Siasa, Uandishi wa Habari za Kiraia, Ubaguzi wa Rangi, Uhuru wa Kujieleza, Utawala, Vita na Migogoro, GV Utetezi
[1]

Shujaat Bukhari, mwandishi wa habari/mtunzi na mhariri mkuu wa Rising Kashmir anayeishi Srinagar. Picha kutoka ukurasa wa Tweeter wa Shujaat Bukhari

Shujaat Bukhari [2], mhariri wa gazeti maarufu la kila siku huko Kashmiri la Rising Kashmir, alipigwa risasi na kufa [3] huko Srinagar, mji wa majira ya joto wa Jammu na Kashmiri na kutuma mawimbi ya mshituko katika ukanda wote.

Gari lake lilizingirwa na watu waliohisiwa kuwa wanamgambo waliompiga risasi yeye na walinzi wake. Walinzi wake wawili walifariki baadaye wakiwa hospitalini kwa sababu ya majeraha.

Wenzake na Bukhari walisema kuwa ndi alikuwa ametka tu nje ya ofisi yake baada ya kumaliza shughuli zake za kila siki na alikiwa anaelekea kufuturu shambulio hilo lilipotokea.

(Onyo: Picha hapo chini kutoka tweeter.)

Bukhari alikuwa kati ya watu wachache wenye ujasiri ndani ya Kashmiri ambao walisimama kati ya India na Pakistani kusuluhisha mgogoro wa Kashmiri.

Soma zaidi: Watu wa Kashmiri dhidi ya watu wa taifa la India [9]

Maandamano ya kudai uhuru (yaliyoitwa “azadi”) na utawala binafsi ndani ya Bonde la Kasmiri yamekuwa hai tangu mwaka 1989, na tangu hapo Jammu na Kashmiri imekuwa chini ya Jeshi la India kwa kifungu cha amri ya Jeshi maalumu lenye silaha [10] na Kifungu cha sheria cha Usalama wa Raia ukiwapa uwanja mpana wa mamlaka. Serikali ya India imetamka rasmi kwamba inaamini kuwa Jammu na Kashmiri sehemu muhimu ya India.

[11]

Polisi wa India akiwa amesimama karibu na chochoro mmoja katika mji wa Srinagar, mji mkuu wa majira ya joto wa Kashmiri unaosimamiwa na India. Picha na mmiliki kupitia Instagram.

Bukhari alifanya kazi na kampuni kubwa za uchapishaji za kitaifa na zile za kimataifa na aliandika makala nyingi zilizogonga vichwa, hakuwai kuona aibu kuchukua msimamo ambao hakuungwa mkono na wengi. Alikuwa mwandishi maalum wa gazeti la Hindu kuanzia mwaka 1997 hadi 2002 na aliendelea kuandikia jarida la Mstari wa Mbele. (Frontline).

Klabu ya Wanahabari ya India imeelezea mshtuko wake [12] na kusikitishwa na tukio hilo lililotokea ndani ya Bonde la Kashmiri.

Chama cha Wahariri wa India kilitoa taatifa yake huko twita [13]:

Salamu za rambirambi zinamiminika kupitia mitandao ya kijamii.

Siddharth Varadarajan, mhariri wa Wire news portal, alitwiti:

Marvi Sirmed, mjumbe wa baraza kuu la Kamisheni na Haki za Binadamu la Pakistani (HRCP) na mwandishi maalum wa Daily Times wa Pakistan, alitwiti:

Hii haikuwa mara ya kwanza Bukhari kulengwa.

Hapo Julai 8, 1996, kikundi cha wanamgambo waliwateka waandishi wa habari 19 katika wilaya ya Anantnag na kuwashikilia kwa masaa saba. Bukhari alikuwa mmoja wao.

Pia alipewa ulinzi na polisi baada ya shambulio dhidi yake hapo mwaka 2000..

Mwanafunzi mwanasiasa Shehla Rashid alitwiti:

Waziri wa zamani wa Jammu na Kashmiri iliyosimamiwa na India, Omar Abdullah, alitwiti:

Kulingana na waandishi wa habari wasio na mipaka, Shujaat Bukhari alisalimika jaribio la kumuua lililofanywa na watu wenye silaha hapo Juni 2006. Shujaat Bukhari aliwaambia [22] Waandishi wa Habari wasio na mipaka kuwa, ” Ni vigumu kutambua ni nani ni maadui zetu na ni nani ni marafiki zetu.”

Pamoja na hili, bunduki haziwezi kuinyamazisha kalamu yake.