Jukwaa Hili Limewasaidia Maelfu ya Wahamiaji Kukutana Tena na Familia Zao Nyumbani

Picha ya kambi ya Wakimbizi Rwanda. Picha na©Elisa Finocchiaro Creative Commons – leseni – BY

Kuna watu wapatao milioni 65 duniani kote kwa sasa ambao wameyakimbia makazi yao. Kamishna Mkuu kwa wakimbizi (UNHCR) anasema hii ni idadi kubwa sana tangu vita ya pili ya dunia. Hali ikiwa ya kutisha hivyo, inavunja moyo zaidi kwa kutambua kuwa wengi wa watu hao wamepoteza mawasiliano na familia zao.

Lakini msaada unaweza kuwa njiani.

Kaka wawili wa Kidenish na wajasiriamali wa mtandaoni David na Christopher Mikkelsen wamepata suluhu ya changamoto hii. Jukwaa lao, REFUNITE, kifupi cha Muungano wa Wakimbizi, limesajili zaidi ya wakimbizi nusu milioni pote duniani na kuwaunganisha na familia zao walizopotezana nazo. Video hii hapa chini inaeleza kwa kifupi kanuni za mradi huu:

Makao makuu ya REFUNITE yako nchini Kenya, lakini mwanzoni yalikuwa nchini Denmarki kwa ushirikiano na Ericsson. Inadhaminiwa na Mfuko wa IKEA na mashirika mengine binafsi na imekuwa na ushirika na muunganiko wa makampuni ya simu za mikononi na Facebook.

Hivyo karibu jumbe milioni 11 zimetumwa kupitia jukwaa hili na utafutaji upatao milioni 9 na usajili wa watu 600,000 kote ulimwenguni. Mpaka 2017 REFUNITE imelenga kusajili wakimbizi milioni moja.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.