Mtu anayejitangaza kuwa nabii, Lethebo Rabalago, amewashtua wa-Afrika Kusini wengi baada ya habari kuenea [2] kuwa anatumia sumu ya wadudu iitwayo Doom, kuponya. Anawanyunyuzia waumini wa kanisa lake sumu hiyo kwenye miili yao na hata kwenye nyuso zao.
Akitangaza nguvu za ‘uponyaji’ zilizoko kwenye sumu hiyo ya Doom, Rabalago aliandika [3] kwenye ukurasa wa Facebook:
Kwa jina langu, mtayatoa mapepo.
Kwa jina nagu, mtashika nyoka. Kila mtakachokishika, kitapata kibali kwa sababu ya upako juu yenu. Sumu ya Doom ni jina tu, lakini unapoisemea maneno inageuka kuwa bidhaa ya kuponyesha. Watu wanaponywa na kufunguliwa kwa kutumia doom. Si kwa uweza wala nguvu, lakini kwa Roho Mtakatifu. Tunampa Mungu utukufu!!
Kampuni inayozalisha sumu hiyo ya wadudu imemshutumu Rabalago na inasema iko kwenye mchakato wa kuwasiliana nae [4] kumuonya kuhusu hatari ya kunyunyuzia sumu ya wadudu ya Doom kwenye nyuso za watu.
Mtandao wa intaneti umeitikia tukio hil kwa hasira, kutokuamini na hata kutengeneza ujumbe wa vichekesho kwa kutumia alama ishara ya #ProphetOfDoom [5] [Nabii wa Doom].
Mtumiaji wa twita anayetumia jina ‘Sound Surgeon’ jalitania:
#ProphetOfDoom [6]
Breaking news: Doom prices have shot up??? pic.twitter.com/mpd3U9HDBG [7]— ?Sound Surgeon? (@speaks_beats) November 22, 2016 [8]
Habari Mpya: Bei ya Doom imepanda
Iloveza aliweka picha hii ikionesha makabati ya kuhifadhia Doom madukani:
Business is good? #Doom [9] #DoomProphet [10] #ProphetofDoom [11] #iloveza [12]❤️?? pic.twitter.com/wzEebVzsvS [13]
— iloveza (@ilovezacom) November 23, 2016 [14]
Biashara [ya Doom] inakwenda vizuri
Mphuma alitaja vitendo vingine vya ajabu vinavyofanywa na manabii hawa wanaojitangaza kila siku nchini Afrika Kusini:
Just when you said you read it enough, petrol, grass, snakes Pastors etc.. now it's happening again. #ProphetOfDoom [6] world coming to an end.
— Mphuma Tshililo (@mphuma27) November 21, 2016 [15]
Pale unapofikiri umesikia vya kutosha, mara wachungaji wa [kunywesha] petroli, [kulisha] majani, nyoka na kadhalika…linatokea jingine jipya. Dunia inaisha.
Matendo ya ajabu ya “kinabii” yanayofanywa na wahubiri wa Afrika Kusini katika miaka ya hivi karibuni ni pamoja na kula majani [16], nyoka [17] and kunywa petroli [16], ambayo inadaiwa hubadilika kuwa juisi ya nanasi baada ya maombi.
Kwa kuzingatia “muujiza” wa hivi karibuni zaidi, Ditjhaba alisema Afrika Kusini inahitaji likizi kidogo:
After this, I think we need a timeout as a country. This is too much and the #prophetofdoom [18] is the last straw. pic.twitter.com/cG4edPGQeH [19]
— Ditjhaba Selemela (@DitjhabaS) November 21, 2016 [20]
Nadhani tunahitaji likizo kama taifa. Hali imezidi kiwango na huyu nabii wa Doom amekomesha kabisa
@shandu009 alitwiti picha ya mtu anayejaribu kuongeza utajiri wake kwenye mashine ya ATM kwa kutumia ushauri wa mchungaji:
#prophetOfDoom [21] pic.twitter.com/BURImBD1MX [22]
— #AlooterContinua✊ (@shandu009) November 24, 2016 [23]
Mtumiaji mwingine wa Twita alisema:
Doom is the answer brothers and sisters lets bow our heads and sPray. #ProphetOfDoom [6]
— Eng TKN (@telferkndumba) November 24, 2016 [24]
Doom ni jibu mabibi na mabwana hebu tuinamishe vichwa tuombe
Vhoni alitania:
Who needs gym when there's doom(Raid)? ?????????????#Prophetofdoom [25] #TrendingSA [26] pic.twitter.com/HTMl69TWRO [27]
— SC&IG @vhoni_henny (@vhoni_henny) November 23, 2016 [28]
Nani anahitaji kwenda kufanya mazoezi wakati kuna Doom?
Mtu mmoja wa Zimbabwe aliweka picha ifuatayo akishauri kuwa rais wa Zimbabwe anahitaji “uponyaji maalumu wa Doom”:
I'll jus leave this here… #prophetofdoom [18] pic.twitter.com/aQqtgDumgt [29]
— Peter Tavaruva (@tavaruva_peter) November 24, 2016 [30]
Ninaachana na suala hili hapa…
Qamatha aliweka picha ya basi ndogo ikiwa na tangazo la Dom akidai linamilikiwa na kanisa hilo:
#ProphetOfDoom [6] just bought a new minibus for congregation. pic.twitter.com/a50YmIwxks [31]
— QAMATHA (@SaAutonomy) November 23, 2016 [32]
Nabii wa Doom amenunua kibasi kipya kwa ajili ya waumini wake
Video ifuatayo inamwonesha nabii akifanya vitu vyake:
Mjasiriamali wa mtandao nchini Afrika Kusini Peter Mansfield alishauri:
LOCK HIM UP, and send congregants for psychiatric examination to determine why they stupid enough to follow him #ProphetOfDoom [6] https://t.co/MutzfJtWSJ [33]
— Peter Mansfield (@Peterman43) November 21, 2016 [34]
MFUNGENI, na wapelekeni waumini wake kwenye matibabu ya akili kujua kwa wamekuwa wajinga kiasi cha kumwamini
Mtumiaji mwingine wa mtandao wa Twita alinukuu kifungu cha biblia kwenye kitabu cha Yohana 3:16. Kifungu hiki kinasomeka: “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanae wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele” :
does one see this doom coming or is it a surprise… #doom [35], #Doompastor [36], #ProphetofDoom [11] pic.twitter.com/YE6ujSR1Wu [37]
— nev.b (@_nevb) 21 de noviembre de 2016 [38]
Hivi kuna mtu anaweza kuona siku ya mwisho ikikaribia au bado mnafikiri itakuja ghafla…
Celeste alifikiri kuwanyunyuzia watu dawa hatari ni kosa la kujaribu kuua:
The #ProphetofDoom [11] should be arrested for attempted murder. #Doom [9] is used to kill so surely the #Hawks [39] or #NPA [40] can whip up a charge.
— Celeste Tema (@celeste_tema) November 21, 2016 [41]
Huyu nabii wa Doom akamatwe kwa kujaribu kukua. Doom inatumika kuua kwa hiyo wanaohusika wafunge washtaka
Kw akutumia picha ya uelimishaji wa mtandaoni nchini Ghana [42], Jake Amo, Barry Roux aliandika:
Dear #ProphetOfDoom [6]
Sorry for the bad handwriting, am writing to ask if Doom can cure TB Joshua. #DoomProphet [10]
Sincerely Your Boy pic.twitter.com/XYZwFNCfh8 [43]
— IG:AdvBarryRoux (@Barry_Roux) November 22, 2016 [44]
Mpendwa Nabii wa Dom, nisamehe kwa mwandiko mbaya, naandika kuuliza kama Doom inaweza kumponya TB Joshua
TB Joshua ni mhubiri wa ki-Naijeria anafahamika kwa kutoa matamshi ya kutabiri. Wakati wa uchaguzi wa Marekani alitabiri kuwa [45] Hillary Clinton angeshinda uchaguzi huo.
Kalabash Media alitumia picha ifuatayo:
Running out of fuel?? …#DoomELA [46] #ProphetOfDoom [6] #DoomProphet [10] pic.twitter.com/RpsMiyCW2i [47]
— Kalabash Media (@KalabashMedia) November 22, 2016 [48]
Umeishiwa mafuta?? Tumia Doom
Rabalago amedai kuwa kwa kutumia nguvu zake za kiroho anaweza kupiga simu bila kutumia kadi ya mawasiliano ya simu [sim card] au hata kuendesha gari bila mafuta.
Mwsiho, unahitaji chupa moja ya Doom ya uponyaji? :
Miracle spray for sale, Contact #ProphetOfDoom [6] prophet Lethebo Rabalago of Kingdom of Doom Church for more details.. pic.twitter.com/mNNJShQAR2 [49]
— IG:AdvBarryRoux (@Barry_Roux) November 24, 2016 [50]
Dawa ya uponyaji unauzwa, wasiliana na Nabii wa doom, Lethebo Rabalago wa Kanisa la Ufalme wa Doom kwa mawasiliano zaidi.
***Katika Kiingereza, Prophet of Doom inaanisha Nabii wa Uongo. Matumizi ya sumu ya Doom yanafanya nabii huyu afahamike kama Nabii wa ‘Doom’, ambayo inaleta maana ya Nabii wa Uongo.