
Vyungu vyenye miguu mitatu vinavyotumika zaidi Botswana. Kama msichana akila chakula kikiwa kwenye chungu, inaaminiwa hataolewa. Picha ya Creative Commons imepigwa na Rach151.
Wa-Afrika, kama watu wengine duniani, hutumia mtandao wa Twita kwa namna mbalimbali. Wakati mwingine ni kwa ajili ya vichekesho. Wakati mwingine ni kutafuta yale yanayofanana kwa nchi na utamaduni tofauti. Wakati mwingine ni yote kwa pamoja.
Kwa mfano, @IGtiz, mwanafunzi wa Kenya, ameanzisha alama ishara ya #100AfricanMyths kujaribu kukusanya imani zinazorithishwa kutoka kizazi kimoja mpaka kingine kwa masimulizi, katika nchi za ki-Afrika.
Imani katika Afrika zinasaidia kukidhi mahitaji tofauti ya kijamii na kiutamaduni. Wazazi, kwa mfano, wanatumia imani hizi kwa ajili ya kuwafuatilia vijana wao.
Hapa ni baadhi ya mifano ya imani za ki-Afrika zinazochekesha.
Faith Mulungi, mtangazaji wa radio nchini Uganda, alitwiti:
When your palms itch,you will receive money#100AfricanMyths
— Faith Liam Mulungi (@Omulungi_Hawt) September 27, 2016
Kiwiko chako kikiwasha, utapokea pesa
@PatohShanqueels alieleza imani maarufu mashuleni wakati wa kuchapwa viboko:
#100AfricanMyths putting Onions under your armpits made you faint when the teacher beat you 😂😂😂😂😂😂
— Soldier ↪ (@PatohShanqueels) September 27, 2016
Kuweka kitunguu kwenye kwapa kunafanya uzimie mwalimu akikuchapa
Usikate kucha zako usiku, kwa mujibu wa @xolelwandengane aliyeko Afrika Kusini:
U can't cut ur nails at night, coz the witches will come and pick them #100AfricanMyths
— Amanda black 🌹 (@xolelwandengane) September 27, 2016
Huwezi kukata kucha zako usiku, kwa sababu wachawi watakuja na kuzichukua
Flo Letoaba, mtangazaji wa redio nchini Afrika Kusini, aliongeza hii kwenye majadiliano hayo:
If you eat out of a pot while cooking, you won't get married #100AfricanMyths
— Flo Letoaba (@florenceletoaba) September 27, 2016
Ukila chakula kikiwa bado kwenye chungu, hutaolewa
Kupiga mluzi usiku kwaweza kuwa hatari —inasemekana:
#100AfricanMyths If you whistle at night, a snake will visit your room
— The Usual Suspect (@Jude_Mugabi) September 27, 2016
Ukipiga mluzi usiku, nyoka atakuja chumbani kwako
Watoto walifundishwa kutokumcheka mlemavu, kwa mujibu wa @NaughtyMilz aliyeko Uganda:
If you laugh at a lame person you would give birth to a lame child…. #100Africanmyths
— ռɨʟօtɨċ (@NaughtyMilz) September 27, 2016
Kama ukimcheka mlemavu unaweza kuzaa mtoto kilema…
Bundi ni mjumbe wa kifo, anasema @iGitz_:
If an owl screechs near your house, someone is gonna die. #100AfricanMyths
— African President👑 (@iGitz_) September 27, 2016
Kama bundi atalia karibu na nyumba yako, basi kuna mtu atafariki dunia
Usiifagilie bahati itoke nyumbani kwako, Vinnie wa Kenya alionya:
Never sweep dirt from your house at night, that is like throwing away luck from your home #100AfricanMyths
— Vinnie (@vinny_wa) September 27, 2016
Usifagie uchafu usiku na ukaotoa nje, kufanya hivyo ni kuitoa bahati nyumbani kwako
Imani hizi zilitumiwa kuwafanya watoto wazingatie masomo:
#100AfricanMyths
Sitting in the front row at school will guarantee you a pass— Tumi Sole (@tumisole) September 27, 2016
Kukaa kwenye mstari wa kwanza shuleni kunakuhakikishia kufaulu
Ingawa imani hizi zimetoka katika sehemu mbalimbali za Afrika, Dickens Jnr, raia wa Marekani mwenye asili ya afrika aishiye Michigan, Marekani anasema amezisikia zote:
Relating to most of the #100AfricanMyths tweets is just 😂. I swear I have heard almost each one Of them.
— Dickens jr (@iickens) September 27, 2016
Hizi imani zote za ki-Afrika zilizosemwa mtandaoni zinachekesha. Haki ya Mungu nimeshazisikia zote