
Shule ya umma nchini Uganda. Watumiji wanasema fedha za walipa kodi zinahitaji kunusuru shule kama hizi. Picha ya Creative Common na The Sustainable Sanitation Alliance.
Pale habari zilipoenea kwamba serikali ya Uganda inakusudia kutumia kiasi cha shilingi za Uganda Trilioni moja (Dola za Kimarekani milioni 300) za walipa kodi kwa ajili ya kunusu biashara kubwa, wa-Ganda walio kwenye mtandao wa Twita waliuita mpango huo kama ‘ufisadi’ na kupendekeza kwamba fedha hizo zingetumika kunusuru shule za umma zilizotelekezwa.
Makampuni ambayo serikali inataka kuyanusuru na mzigo wa madeni makubwa yaliyotokana na mikopo iliyochukuliwa kutoka kwenye mabenki mbalimbali nchini Uganda. Biashara nyingi zinaendeshwa na wafanyabiashara wakubwa wenye nguvu. Baadhi ya maafisa wa benki kuu na wizara ya fedha wamepinga mpango huo.
David Mpanga, mwanasheria wa Uganda, aliuita mpango huo kuwa ni ‘kuwafanya wananchi walipe hasara':
The privatisation of profit and socialisation of loss. Must we all pay for business failure when we didn't all share in the profits made?
— David F.K. Mpanga (@dfkm1970) July 22, 2016
Kubinafsisha faida na kuchangia hasara. Lazima wote tugharamie hasara ya biashara za matajiri lakini lini tulichangia faida wanayopata?
Allan Ssenyonga alishangazwa nkufahamu kwamba mmoja wa makampuni yaliyoorodheshwa kuingia kwenye mpango huo ni biashara ya manyoya:
Club Silk is one of the companies in need of a bail out. Is this really a priority for Uganda?? #ScamBailOuts
— Allan Ssenyonga (@ssojo81) July 22, 2016
Club Silk ni moja wapo ya makampuni yanayohitaji kunusuriwa. Hivi kweli hiki ni kipaumbele kwa Uganda?
Fredrick Tumusiime alipendekeza:
For any #bailout, the public must acquire a stake in the firm(s). No public money for private sins. #ScamBailOuts https://t.co/kQ95Ky2cqB
— Fredrick Tumusiime (@tufre80) July 22, 2016
Ili hatua zozote za kutoa ruzuku kwa makampuni zifanyike, lazima wananchi wawe na hisa kwenye kampuni husika. Fedha za umma zisitumike kugharamia dhambi za watu binafsi
Wa-Ganda walihoji umuhimu wa mipango hiyo ya kuwasaidia wafanyabiashara wakubwa wenye uhusiano na wanasiasa nchini humo wakati serikali ikiwekeza kidogo sana kwenye miundombinu, shule na huduma za afya.
Sarah Bireete alipendekeza kwamba serikali inusuru shule za umma zenye hali mbaya:
Poor Ugandans can't continue to subsidise the rich #ScamBailOuts Bailout schools with no classrooms, books &latrines pic.twitter.com/YkNYlFEQd1
— Bireete Sarah (@SarahBireete) July 23, 2016
Wa-Ganda masikini wanaendelea kutoa ruzuku kwa matajiri. Kwa nini tusiziokoe shule zisizokuwa na madarasa, vitabu na vyoo?
Jeff aliweka picha ya kampuni moja ambayo alifikiri serikali ingeweza kuisaidia kumaliza madeni yake:
A photo representing the companies that need bail out by the Government using taxpayers money #ScamBailOuts pic.twitter.com/nZuldcEzBH
— Jeff 4.7.1™ (@andsjeff) July 23, 2016
Picha inaonesha ‘kampuni’ ambayo inahitaji sana kupata msaada wa fedha za walipa kodi
Picha nyingine ya shule ya umma yenye hali mbaya:
Karungu Seed School,Buhweju District.
Does it need a BailOut? NO,Bailout companies that don't pay Tax #ScamBailOuts pic.twitter.com/giwY9J1zXa
— Jeff 4.7.1™ (@andsjeff) July 23, 2016
Shule ya Msingi Karungu, Wilaya ya Buhweju. Hivi shule hii haihitaji msaada? Hapana, tusaidie makampuni ambay0 hata hivyo yanakwepa kodi
Wakati huo huo Samwise Gamgee alishauri:
If Bailing them out is a matter of National Importance, sharing their profits should be a matter of National Importance too. #ScamBailouts
— Samwise Gamgee (@Sambannz) July 22, 2016
Kama kutoa msaada kwa makampuni haya ni suala lenye Maslahi ya Taifa, kutoa faida yanayopata makampuni hayo ni suala lenye Maslahi ya Taifa pia