Kuna tovuti ya picha inayoitwa wanadamu wa New York (Humans of New York [1]) ambayo imehamasisha kuweko kwa wanadamu wa Kibera ama (Humans of Kibera [2]). Huu ni mradi [3] wa Mtandao wa Habari wa Kibera (KNN), kikundi cha waandishi vijana wa habari kutoka Kibera, Nairobi, Kenya. Mradi huu unatuonyesha vyema maisha ya wakazi wa Kibera [4]—makazi duni yaliyo kubwa zaidi Kenya—kwa mtandao wa Tumblr [2].
Hizi ni picha kadhaa zinazosimulia maisha ya Wanadamu wa Kibera:
Mnamo mwaka wa 2012 katika Mkutano wa Mkuu wa Global Voices Nairobi, Rising Voices ikishirikiana [18] na Mfuko wa Kibera na Mtandao wa Habari wa Kibera iliwakutanisha waandishi wa Global Voices na wanajamii wa Kibera kujaribu kushiriki shughuli za uandishi wa kiraia katika eneo la Kibera.