‘Escopetarra': Chombo cha Kipekee

Kama unaamini kuwa hakuna jambo zuri linaloweza kutokana na bunduki aina ya gobore, basi unapaswa kukifahamu kifaa kiitwacho “escopetarra”— mchanganyiko uliotokana na kubadilisha silaha mbili “hatari” (an AK-47 na gitaa) na kuwa kifaaa cha amani. “Escopetarra” ni neno lililotokana na muunganiko wa maneno ya Kispaniola, “escopeta” (bunduki) na “guitarra” (gitaa).

Kwenye podikasti yake katika lugha ya Kispaniola, mwanamuziki wa Colombia, César López anazungumzia namna alivyokibuni chombo hiki tokea alipopata wazo hadi kwenye mambo yote ya kiufundi aliyokabiliana nayo, pamoja na sauti ya chombo hiki.

Duniani kuna silaha nyingi sana aina ya AK-47s kuliko aina nyingine yoyote, na inashangaza kwa namna silaha hii ilivyo nafuu kuitengeneza. Inakadiriwa kuwa kuna idadi ya AK-47 zinazokadiriwa kufika milioni 35-hadi-50, na bila kuhesabu zile zinazotengenezwa kinyemela kila mwaka.

“Primero, el AK 47 es el arma que más muertos le ha causado al planeta Tierra en toda su historia. Es el arma que se ha usado en Sudáfrica, Medio Oriente, Centro América, en Colombia”, dijo López en entrevista con la cadena estadounidense Univision.

“Awali ya yote, AK-47 ndiyo silaha iliyosababisha idadi kubwa zaidi ya vifo kuliko silaha nyingine yoyote duniani. Inatumika Afrika ya Kusini, Mashariki ya Kati, Amerika ya Kusini, na pia Colombia.”, alisema López katika mahojiano na Mtandao wa Televisheni ya Marekani,Univision.

Un
“Escopetarra” ya kwanza ilitengenezwa mwaka 2003 kwa kutumia bunduki aina ya Winchesta  pamoja na gitaa la umeme aina ya Stratokasta . Kinachofanyika ni kuwa, bunduki hufumuliwa kwa namna ambayo haiwezi kuchukuliwa tena kama silaha na wala kutumiwa kwa matumizi ya namna hiyo.

Hadi sasa, kuna takribani “escopetarra” 20 ambazo zimeshakabidhiwa kwa wanamuziki mashuhuri pamoja na viongozi wa kimataifa wanaotetea amani ikiwa ni pamoja na bendi ya Colombia inayofahamika kama, Aterciopelados, mwanamuziki wa Argentina, Fito Páez, pamoja na UNESCO.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.