- Global Voices in Swahili - https://sw.globalvoices.org -

Ramani Hizi Zaonesha Mahali Walipotesewa na Kuuawa Wanahabari wa Kambodia

Mada za Habari: Asia Mashariki, Kambodia, Haki za Binadamu, Maandamano, Siasa, Uandishi wa Habari za Kiraia, Uhuru wa Kujieleza, Utawala, Vyombo na Uandishi wa Habari

harassment_of_media_cambodia [1]Kituo cha Haki za Binadamu cha kambodia kimezindua jarida [2] linaloelezea ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa kwa waandishi wa habari nchini Kambodia. Katiba ya nchini Kambodia inatoa uhuru wa kupashana habari lakini wanahabari wanazidi kunyanyaswa na kuuawa, hususani kwa waandishi wanaopasha habari kuhusiana na ukiukwaji wa maadili unaofanywa na maafisa wa serikali pamoja na upashaji habari wa masuala ya kibiashara yanayohusishwa na viongozi wakubwa serikalini.