Kuhusu Uamuzi wa Mahakama wa Haki ya Kusaidiwa Kufa Nchini Afrika Kusini

Profesa Pierre de Vos anaingia rasmi kwenye mjadala mkali kuhusu uwezekano wa kumsaidia mtu kufa nchini Afrika Kusini baada ya Mahakama Kuu nchini humo kuamua kwamba mtu anayekufa ana haki ya kusaidiwa kufa na daktari ili aweze kuyahitimisha maisha yake:

Ni muhimu kuona kwamba hukumu hii haimlazimishi mtu kuyakatisha maisha yake au kumsaidia mtu kufanya hivyo. Hilo bado linabaki kuwa uamuzi wa mtu binafsi. Hukumu hii inaweka msisitizo wa sheria ya makosa ya jinai (au, ningeongeza, sheria ya maadili ya Baraza la Watumishi wa Sekta ya Afya Afrika Kusini [HPCSA] kwamba haiwezekani kutekeleza jambo lolote lililo kinyume na misimamo ya kidini au kimaadili kwa mtu yeyote. Hata hivyo, hayo haiwalazimishi wale wenye imani hizo kuweza kuvunja imani zao wenyewe.

Zaidi, kama Mahakama ya Katiba itapitisha hukumu hiyo basi itafaa kwa Bunge kupitisha mfumo utakaowalinda wagonjwa. Bila sheria hizo mgonjwa atapaswa kwenda mahakamani kupata ruhusa ya kusaidiwa kufa.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.