Umoja wa Ulaya Hautatoa Nafuu ya Kodi ya VAT kwa Vitabu ya Kidigitali

Imagen compartida por Blog de sinerrata editores    usada con permiso

Bendera ya Umoja wa Ulaya. Picha ya Sinerrata Editores, imetumiwa kwa ruhusa.

Mnamo Machi 5, 2015, Mahakama ya Haki ya Umoja wa Ulaya ilitoa hukumu kwamba punguzo la kodi ya ongezeko la thamani (VAT) lililotolewa kwa vitabu vinavyochapishwa halitahusisha vitabu vya kidijitali, kwa kuzingatia kwamba kila kinachosambazwa au kutolewa kwa mfumo wa kieletroniki au kwa mtandao wa intaneti ni huduma. Amalia Lopez anahoji hukumu hiyo kwenye blogu ya Sinerrata Editores:

Lo que más me ha llamado la atención es que refuerzan la decisión utilizando el argumento del soporte, […] que igual tuvo sentido en algún momento del pasado pero hoy en día me resulta completamente absurdo. Es verdad, el libro electrónico es un archivo no un objeto pero, ¿es un libro menos libro porque lo guardo en mi ordenador o mi lector electrónico en vez de en la estantería? ¿Cuándo leo un libro digital la experiencia cultural es menor que cuando es un libro de papel? Es decir, lo que este tribunal ha sentenciado (o esa es mi interpretación) es que lo que hace de un libro un producto cultural y por tanto merecedor de un impuesto reducido (y un menor coste para los consumidores) es el papel en el que está impreso.

Kinachonishangaza ni kwamba walitumia mfumo wa kitabu kama hoja ya kufanyia maamuzi yao, […] jambo linaloweza kuwa na mantiki kwa kipindi cha nyuma, lakini leo, ninaona huu ni sawa na upuuzi. Ni kweli, kitabu cha kidijitali ni faili tu na sio kitu, lakini je nikikiweka kitabu kwenye kompyuta yangu au kifaa kingine cha kukisomea badala ya kukiweka kwenye kabati, hiyo inakifanya kisiwe na hadhi ya kitabu? Ninapokisoma kitabu kilicho kwenye mfumo wa kidijitali, uzoefu wa kitamaduni ninaoupata unakuwa pungufu ya ule ninaoupata nikiwa nakisoma kitabu kwenye karatasi? Ndio kusema, kilichoamuliwa na mahakama (au, angalau, hiyo ni tafsiri yangu tu) ni kwamba kinachofanya kitabu kiwe zao la utamaduni, na hivyo kustahili kupata punguzo la kodi (na hiyo maana yake ni punguzo la bei kwa wateja), ni karatasi linalotumiwa kuchapishia kitabu hicho.

Uamuzi huo unahusisha vitabu vinavyopakuliwa au kutazamwa mtandaoni na inahusisha mifumo kama kompyuta, simu za kisasa na vifaa vingine vya kusomea.

Unaweza kusoma zaidi kuhusu mada hii kwenye makala ya  Amalia Lopez kwenye mbogu ya Sinerrata Editors, na kuwafuatilia kwenye mtandao wa Twita: @Sinerrata.

Makala haya ni sehemu ya 43 ya #LunesDeBlogsGV (Jumatatu ya Blogu kwenye GV) mnamo Machi 2, 2015.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.