Mwizi Akamatwa, Aomba Msamaha na Kusamehewa

Captuira de pantalla de video en YouTube del usuario KDNA15TV.

Picha ya video kwenye mtandao wa YouTube iliyowekwa na mtumiaji KDNA15TV.

Labda alidhani ingekuwa vyepesi kuiba shampoo mali ya mmiliki wa duka nchini Peru, lakini mambo yalimwendea mrama mwizi huyu.

Mtu mmoja akiwa ameongozana na mwenzake waliingia kwenye duka lililoko kwenye jiji la Huancayo nchini Peru, wakisema walikuwa wanataka kununua pombe, na mmiliki alipokuwa amepumbazwa kidogo, jamaa walibeba boksi la shampoo. Mmiliki aligundua mchezo wao na kuwaarifu walinzi. Ili kuzuia tukio hilo lisifike mbali, mmoja wa wezi hao alipiga magoti na kuomba msamaha. Mmiliki wa duka, aliyekuwa mwanamke, aliguswa na kitendo hicho na akaamua kuachana na mpango wa kuwachukulia hatua. Mwenzake na mwizi huyo aliyeomba msamaha naye alinufaika na msamaha huo, ingawa hakuwa ameomba msamaha.

Jamaa huyo alidai hatarudia tena kufanya kitendo kama hicho.

Blogu ya Noticias Huancayo Perú ilisimulia mhutasari wa tukio hilo:

Se arrodilló y pidió perdón a la anciana manifestando que era la última vez que robaría. La agraviada […] al aceptar sus súplicas del ladrón negó en denunciar el hecho.

Lipiga mgoti na kumwomba mwanamke wa umri wa makamo amsamehe, akimsihi kwamba hiyo ndiyo itakuwa mara yake ya mwisho kuiba. Mama huyo […] kwa kukubali ombi la mwizi wake, aliamua kuachana na mpango wa kutoa taarifa ya tukio hilo.

Mtumiaji KDNA15TV aliweka video zinazozungumzia tukio hilo:

Mwizi apata msamaha baada ya kupiga magoti kuomba msamaha kwa kuiba boksi la shampoo. Alikuwa na rafiki yake waliyekuwa wameambatana…

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.