Kulinda Taarifa Binafsi Nchini Ajentina Bado Kuna Safari Ndefu

Cloud Computing - Photo by Quinn Dombrowski on Flickr. (CC BY-NC-SA 2.0).

Ulinzi wa taarifa za kompyuta – Picha na Quinn Dombrowski kwenye mtandao wa Flickr. (CC BY-NC-SA 2.0).

Kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya gazeti la mtandaoni Haki za Kidijitali: Amerika Kusini & Visiwa vya Caribbean, No.21Mmwanasheria wa ki-Ajentina Valeria Milanés anaeleza kwamba hata kama Marekani ni kiranja wa dunia kwenye kuchakata taarifa (data), bado haina sheria ya kulinda taarifa za watu. Marekani pia inachukuliwa kama nchi yenye “kiwango kisichofanana cha ulinzi kwenye viwango vya kitaifa na kimataifa.”

Bahati mbaya, katika bara la Amerika Kaskazini na nchi nyingine, mabadiliko ya teknolojia yamezidi kwa mbali kutengenezwa kwa sheria zinazodhibiti matumizi yake. Milanés anaeleza hali ilivyo nchini Ajentina na kuitaja Kurugenzi ya Taifa ya Kulinda Taarifa za watu na Sheria ya Taarifa Binafsi, D.N.P.D.P., (Sheria 25.326 na 26.343), ambayo ni kati ya “masuala muhimu zaidi ya ulinzi wa taarifa.” Tatizo ni utekelezaji wake:

…en 2012, y luego de doce años de funcionamiento, la D.N.P.D.P. tenía registradas 20.000 bases de datos, contra 1.600.000 que tenía registradas a la misma fecha y en similar plazo la Agencia Española de Protección de Datos.

…mwaka 2012, baada ya miaka kumi na mbili ya utekelezaji, taasisi ya D.N.P.D.P. imeandikisha ‘database’ 20,000, ukilinganisha na ‘database’ 1,600,000 zilizoandikishwa katika kipindi hicho hicho na Wakala wa Ulinzi wa Taarifa nchini Uhispania.

Milanés anasema kwamba mfumo wa kulinda taarifa kwenye kompyuta unaleta changamoto mpya:

…las grandes empresas multinacionales prestadoras de los servicios de nube pública se caracterizan por utilizar contratos de adhesión, que por lo general no contienen las especificaciones requeridas en la ley 25.326 y en los que hasta la ley aplicable y jurisdicción prefijada corresponde al país en los que estas empresas tienen sus domicilios legales –por lo general, ciudades de Estados Unidos–. Es más, inclusive los servidores en los que se almacena la información pueden no encontrarse en Argentina.

…lwatoa huduma wakubwa wa kimataifa wanaolinda taarifa za watumiaji wnaafahamika kwa kuheshimu mikataba, ambayo mara nyingi huwa na masuala mahususi yenye misingi ya Sheria 25.326 na ambayo sheria zinazotumika na mamlaka ya kisheria ni yale ya nchi ambazo makampuni hayo yanatoka, na mara nyingi ni miji ya Marekani. Zaidi, hata vifaa vya kuhifadhia taarifa [servers] mara nyingi hazipo nchini Ajentina

Kwa hiyo, uzoefu wa wa-Ajentina hautofautiani na ule wa nchi nyingine kwenye ukanda wa Amerika Kusini, pamoja na kuwa na sheria za kulinda taarifa binafsi na makampuni bado safari ni ndefu.

Milanés anahitimisha kwa kusema kwamba suala hili linahitaji “kuchukua hatua za utekelezaji adhubuti unaoendana na sheria za sasa na kutumika kwa mifano bora ya kibiashara inayoruhusu, kwa kiasi kikubwa, faragha ya taarifa binafsi na kutoa uhakika wa usalama unaotakikana.”

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.