‘Kulea Mtoto Ukiwa Mtoto': Idadi Kubwa ya Mimba za Utotoni Nchini Venezuela

Desireé Lozano, anayeblogu kwenye blogu ya Voces Visibles, anatoa mwito kwa ongezeko kubwa la mimba za utotoni nchini Venezuela, ambapo asilimia 25 ya mimba ni za vijana, na kukosekana kwa sera sahihi za kudhibiti tatizo hili na matokeo yake. Takwimu za Venezuela zinaonesha kwamba nchi hiyo ina idadi kubwa ya mimba za utotoni barani Amerika ya Kusini na imekua ya kwanza kwa miaka miwili iliyopita.

Vifo vya watoto ni suala kuu linalohusiana moja kwa moja na mimba za utotoni. Desiree anamtolea mfano Dinorah Figuera, makamu wa rais wa Kamati ya Bunge inayoshughulika na Familia aliyesema kwamba wajibu wa serikali ni kuzuia mimba hizo:

“Una de esas consecuencias es que las madres adolescentes son mujeres que pierden oportunidades para desarrollarse desde el punto de vista profesional y aceptan cualquier tipo de trabajo para tener algún tipo de ingresos. Por esta razón el Estado debe aplicar una gigantesca campaña de concientización para la prevención del embarazo adolescente”, señala la diputada venezolana

“Matokeo moja wapo ya kuwa mama katika kipindi cha utoto ni mwanamke kukosa fursa za kujiendeleza kitaaluma, na hivyo kujikuta akifanya kazi yoyote ile kujipatia kipato. Kwa sababu hii, serikali lazima ifanye kamepni kuba kuzuia mimba za utotoni,” alisema.

Kwa nyongeza, mimba za utotoni zinachangia kuongezeka kwa umasikini wa kipato kwa wanawake. Zaidi, hali hii inaleta hatari kwa afya ya mama, hatari kubwa kuliko kawaida. Kwenye makala yake, mwandishi anakusanya matamshi mbalimbali ya wataalamu kuhusu suala hilo na hivyo kutoa mwanga kuhusiana na tatizo hilo.

Endele kusoma kazi za Desireé Lozano na Voces Visibles hapa au kwenye mtandao wa Twita.

Makala haya ni ya 46 kwenye mfulululizo wetu wa #LunesDeBlogsGV  (Jumatatu ya Blogu GV) mnamo Aprili 13, 2015.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.